KIKOSI CHA UFARANSA CHAKAMATA MELI ILIYOJAA SILAHA ZINAZOPELEKWA SOMALIA

Kikosi cha askari cha majini cha Ufaransa kinachofanya dori kaskazini mwa bahari ya India kimeikamata meli iliyojaa sialaha zinazosemekana zilikuwa zinapelekwa nchini Somalia.

Mamia ya bunduki zikiwemo aina ya machine gun pamoja silaha za makombora zimekutwa kwenye meli hiyo.

Silaha zilizokamatwa zipo katika orodha ya zilizopigwa marufuku na Umoja wa Mataifa kuingia mikononi mwa makundi ya wapiganaji wa Somalia.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni