PAKISTANI WAOMBOLEZA VIFO VYA WATU 70 VYA SHAMBULIO LA BOMU

Wananchi wa Pakistani wanaomboleza vifo vya watu 70, vikiwemo vya watoto 29 vilivyotokea katika shambulizi la Jijini Lahore.

Serikali ya Mkoa wa Lahore imetangaza siku tatu za maombolezo, na siku moja ya maambolezo imetangazwa katika maeneo mengine Pakistani.

Kundi lililojitenga kutoka kwa Taliban la Jamaat-ul-Ahrar limekiri kufanya shambulizi hilo lililowalenga Wakristo waliokuwa wakisherehekea Sikukuu ya Pasaka, ambapo watu 300 walijeruhiwa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni