Mkurugenzi
 Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA), Dkt. Ally Simba akielezea
 matumizi ya intaneti yalivyo nchini na changamoto zinazowakabili 
watumiaji wa huduma hiyo. 
Mwaka 
2016 unakuwa mwaka wa neema kwa Tanzania kupata fursa ya kuandaa Mkutano
 unaowakutanisha wadau wa intaneti (African Peering and Interconnection 
Forum), mkutano unaotaraji kufanyika Agosti 31 – Septemba 1, jijini Dar 
es Salaam.
Akizungumzia
 mkutano huo, Meneja Mwandamizi wa Maendeleo wa Taasisi ya Internet 
Society, Michuki Mwangi amesema mkutano huo unalengo wa kukutanisha 
wadau mbalimbali wa intaneti ili kutanua miondombinu ya intaneti katika 
bara la Afrika.
Amesema
 taasisi yake inapenda kuona huduma ya intaneti ikipatikana kwa urahisi 
kwa watumiaji wake Afrika na hivyo kupitia mkutano huo wataweza kutazama
 jinsi gani wanaweza kushirikiana na kubadilishana takwimu za watumiaji 
wa mitandao kwa bara zima la Afrika.
“Tunatambua
 kuwa watumiaji wa intaneti wanazidi kuongezeka na kupitia mkutano huu 
tutaweza kuangalia jinsi gani tunaboresha huduma ya intaneti iwe bora 
ili iweze kutumiwa na watu wengi zaidi,” amesema Mwangi.
Nae 
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA), Dkt. Ally Simba
 amesema mkutano huo una umuhimu kwa Watanzania kwa kupata fursa ya 
kujifunza na kubadilishana mawazo na watu kutoka mataifa mengine katika 
huduma ya intaneti.
Amesema
 kwa sasa Tanzania bado ina changamoto nyingi katika huduma ya intaneti 
na kupata nafasi hiyo ya kuandaa mkutano kutakuwa na faida kwa mashirika
 yanayotoa huduma ya intaneti ili kuwawezesha kutambua ni jinsi gani 
wataboresha huduma kwa wateja.
“Nchi 
yetu inawatumiaji wengi wa intaneti ila bado kuna changamoto nyingi 
ikiwepo usalama wa mtandao na serikali inafanya jitihada nyingi kumaliza
 changamoto hizo na kupitia mkutano huu tunaamini utasaidia zaidi 
Watanzania kupata kitu kipya katika huduma ya intaneti,” amesema Simba.
Kwa 
upande wa Mwenyekiti wa TISPA, Vinay Choudary amesema Watanzania wengi 
bado hawajafahamu umuhimu wa intaneti kutokana na kutokuwa na ujuzi wa 
kutosha kuhusu intaneti lakini kupitia mkutano huo ulioandaliwa na 
Internet Society wataweza kuapata elimu mpya kuhusu intaneti.
Mkurugenzi
 Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA), Dkt. Ally Simba (kushoto)
 akizungumza jambo na Mwenyekiti wa TISPA, Vinay Choudary.
Wa 
kwanza kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini 
(TCRA), Dkt. Ally Simba (kushoto), Mwenyekiti wa TISPA, Vinay Choudary, 
Meneja Mradi wa Tanzania Internet Exchange (TIX), Frank Habicht na 
Meneja Mwandamizi wa Maendeleo wa Taasisi ya Internet Society, Michuki 
Mwangi wakizungumza jambo kabla ya kuanza kwa mkutano huo.
Mwenyekiti wa TISPA, Vinay Choudary akifungua mkutano huo.
Meneja
 Mwandamizi wa Maendeleo wa Taasisi ya Internet Society, Michuki Mwangi 
akizungumzia mkutano wa Intaneti, AfPIF utakaofanyika nchini, Agosti, 30
 - Septemba, 1
Baadhi ya washiriki waliohudhuria mkutano huo.
Baadhi ya waandishi waliohudhuria mkutano huo.
Washiriki wakiwa katika picha ya pamoja.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni