Waziri
 wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akizindua rasmi 
albam mpya ya mwimbaji Goodluck wakati wa tamasha la Pasaka 
lililofanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza leo na 
kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Mwanza , Wabunge pamoja na
 Maaskofu wa makanisa ya Mwanza.
Tamasha
 hilo ambalo limehudhuriwa na mashabiki wengi mkoani humo limetumbuizwa 
na waimbaji mbalimbali wa nyimbo za injili kutoka hapa nchini na nchi 
jirani za Zambia na Kenya, waimbaji hao ni Upendo Nkone , Martha baraka ,
 Jesca BM, Joshua Mlelwa , Tumsifu Rufutu, Christopher Mwahangila, 
Jeniffer Mgendi, Bonny Mwaiteje, Goodluck ambaye amezindua albam yake 
mpya na waimbaji Faustine Munishi kutoka nchini Kenya, Solomon Mukubwa 
kutoka Nchini Kenya pamoja na Ephraim Sekereti kutoka nchini Zambia wote
 kwa pamoja wamefanya maonesha mazuri yaliyopagawisha mashabiki wa 
muziki wa injili katika uwanja wa CCM Kirumba na kuwafanya wacheze kila 
wakati, katika picha kulia ni mwimbaji Goodluck na kushoto ni Bw. Alex 
Msama Mkurugenzi wa kampuni ya Msama Promotion inayoandaa matamasha 
hayo.
Tamasha
 hilo litaendelea kesho kwa onesho kabambe linalotarajiwa kufanyika  
mjini Kahama mkoani Shinyanga baada ya kumaliza maonyesho  mawili katika
 mikoa ya Geita na Mwanza.(PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE-MWANZA)
Waziri
 wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye wa nne kutoka 
kulia  akimsikiliza Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mh. John Mongela alipokuwa 
akimkaribisha rasmi ili kutoa salam zake kutoka kwa serikali.
Waziri
 wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akishiriki katika
 sala maalum ya kuombea albam ya mwimbaji Goodluck  wa pili kutoka kulia
 iliyotolewa na maaskofu wa mwanza kabla ya kuizindua
Waziri
 wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akishuka kutoka 
jukwaani kwa ajili ya kuizindua rasmi albam hiyo na kutoa salaam za 
serikali katika tamasha la Pasaka.
Mkuu
 wa mkoa wa Mwanza Mh. John Mongela akipokewa na Mkuu wa wilaya ya 
Nyamagana Mh. Baraka Konisaga kushoto na Mkurugenzi wa Msama Promotion 
Bw. Alex Msama wakati alipowasili kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini 
Mwanza.
Mkuu
 wa wilaya ya Nyamagana Mh. Baraka Konisaga akipokewa  na Mkurugenzi wa 
Msama Promotion Bw. Alex Msama wakati alipowasili kwenye uwanja wa CCM 
Kirumba jijini Mwanza.
Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza Ndugu Miraji Mtaturu akiinunua albam ya mwimbaji Goodluck mara baada ya kuzinduliwa rasmi na Waziri
 wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye kwenye tamasha la
 Pasaka lililofanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Waziri
 wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akitoa salam zake
 na kukemea watu wanaojihusisha na wizi wa kazi za wasanii na kusema 
serikali ya awamu ya tano itahakikisha wahusika wote wanashughulikiwa 
vya kutosha ili kuhakikisha wasanii wanapata haki yao katika kazi zao na
 jasho lao.
Mwimbaji
 Goodluck akiimba mara baada ya kuizindua rasmi albam yake kwenye 
tamasha la pasaka jijini Mwanza lililofanyika kwenye uwanja wa CCM 
Kirumba.
Mwimbaji Upendo Nkone akifanya vitu vyake jukwaani na kuwarusha vya kutosha mashabiki waliohudhuria katika tamasha hilo.
Waziri
 wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akiongoza na 
viongozi mbalimbali pamoja na baadhi ya maaskofu kucheza wakati mwimbaji
 Upendo Nkone alipokuwa akiimba jukwaani.
Waziri
 wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akipiga picha ya 
pamoja na waimbaji wa muziki wa injili mara baada ya tamasha hilo 
kumalizika kutoka kulia ni Bonny Mwaiteje. Jesca BM  na Upendo Nkone.
Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akicheza wakati mwimbaji Bonny Mwaiteje alipokuwa akitumbuiza.
Mwimbaji Bonny Mwaiteje akifanya vitu vyake jukwaani
Mkuu
 wa wilaya ya Nyamagana Mh. Baraka Konisaga akipunga mkono huku akicheza
 na baadhi ya viongozi wa mkoa wa Mwanza na maaskofu pamoja na 
wachungaji wakati mwimbaji Upendo Nkone akifanya vitu vyake jukwaani.
Roho
 wa Bwana Yesu akiwashukia mashabiki wa muziki wa injili wakiwa 
wamenyanyua mikono yao juu juu wakati mwimbaji Upendo Nkone alipokuwa 
akiimba jukwaani.
Alex Msama Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion pamoja na Mkewe wakielekeakuketi jukwaa kuu.
Waziri
 wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akipokelewa na 
Alex Msama na Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mh. John Mongela alipowasili uwanja
 wa CCM Kirumba.
Mwimbaji Martha Baraka akitumbuiza katika tamasha hilo.
Naye Mwimbaji Jeniffer Mgendi akafanya mambo makubwa jukwaani kama anavyoonekana.
Bw. Alex Msama kulia akiwa na Mkewe katikati pamoja na MC wa matamasha ya Pasaka MC Mwakipesile.
Mmoja wa washabiki ambaye ni mlemavu alishindwa kujizuia akaamua kucheza kama anavyoonekana katika picha.
Mwimbaji Joshua Mlelwa amefanya mambo makubwa jukwaani katika tamasha hilo kama kawaida yake.
Mashabiki wakicheza kwa furaha katika tamasha hilo.
Mwimbaji Faustine Munishi kutoka nchini Kenya akipagawisha mashabiki na nyimbo zake za kuabudu kama vile "Malebo".
Mwimbaji Christopher Mwahangila akiwapa upako mashabiki kupitia injili ya uimbaji.
Mwimbaji Ephraimu Sekereti kutoka nchini Zambia naye akaimba nyimbo za kusifu na kuabudu.
Solomon Mukubwa akiafunga kazi na nyi,bo zake kali zilizowafanya mashabiki kuwa wima wakati wote kama wanavyoonekana.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni