Wafanyakazi
 wa kiwanda cha TBL cha Arusha wakifanya mazoezi ya kukimbia wakati wa 
uzinduzi wa kampeni ya Afya Kwanza mwishoni  mwa wiki 
Meneja
 wa kiwanda cha TBL mkoa wa Arusha,Salvatory Rweyemamu akipiga mpira 
kuashiria kuanzishwa kwa kampeni ya Afya Kwanza iliyoanzishwa na TBL 
Group kwa lengo la kuimarisha afya za wafanyakazi wake. 
  
 Meneja Uendeshaji wa taasisi ya AAR Insurance Tanzania Ltd, Dk Harold 
Adamson akizungumza na wafanyakazi wa kiwanda cha TBL mkoa wa Arusha juu
 ya umuhimu wa kuimarisha afya zao kwa kufanya mazoezi wakati wa 
uzinduzi wa kampeni ya Afya Kwanza uliofanyika kiwandani hapo mwishoni 
mwa wiki.
Wafanyakazi
 wa TBL kiwanda cha Arusha wakimsikiliza mtaalamu wa lishe huku 
wakijipatia matunda  baada ya kufanya mazoezi ya kuimarisha viungo vyao 
wakati  wa uzinduzi wa kampeni ya Afya Kwanza iliyofanyika kwenye 
kiwanda hicho eneo la Themi jijini Arusha mwishoni mwa wiki. 
………………………………………………
Kampeni ya TBL Group imezindua 
kampeni ya kuimarisha afya za wafanyakazi wake wote ambapo wanashiriki 
kufanya mazoezi ya mwili sambamba na  kupatiwa  kupatiwa elimu 
inayohusiana na lishe bora na matumizi ya vyakula visivyo na athari.
Afya Kwanza ambayo imeanzia kwa 
wafanyakazi waliopo Makao makuu na viwanda vilivyopo jijini Dar es 
Salaam mwishoni mwa wiki imezinduliwa katika kiwanda cha Arusha na 
kushirikisha wafanyakazi wa kiwanda hicho.
Msimamizi wa Programu hii ,Julieth
 Mgani alisema kuwa itakuwa endelevu na wafanyakazi wameonekana 
kuifurahia katika kipindi cha muda mfupi tangia ianzishwe.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni