Rais
 wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli 
akizungumza mbele ya Waku wa Mikoa mara baada ya kuwaapisha leo Ikulu 
jijini Dar.Rais Dkt Magufuli amewapa siku 15 Wakuu wa Mikoa kuwaondoa 
watumishi hewa walio katika orodha ya malipo ya mishahara ya watumishi 
wa umma katika Mikoa yao.Picha na Michuzi Jr-MMG
Na Jacquiline Mrisho- Dar es salaam.     
Rais
 wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli 
amewapa siku 15 Wakuu wa Mikoa kuwaondoa watumishi hewa walio katika 
orodha ya malipo ya mishahara ya watumishi wa umma katika Mikoa yao.
Rais
 Dkt. Magufuli amesema hayo leo Ikulu Jijini Dar es salaam baada ya 
kuwaapisha Wakuu wa Mikoa aliowateua Machi 13 mwaka huu ambapo 
amewaagiza washirikiane na Wakurugenzi wa Halmashauri kuwaondoa 
watumishi hewa.
“Nimewapa
 siku 15 kuanzia leo mkashirikiane na Wakurugenzi wa Halmashauri zenu 
kuwatoa wafanyakazi hewa, nikigundua kuwa bado kuna wafanyakazi hewa, 
Mkurugenzi husika atafukuzwa kazi na atapelekwa mahakamani”,
Na
 kusisitiza “Nimeamua kuwachagua nikiamini kwamba mtaniwakilisha vizuri 
katika Mikoa yenu, nawaomba mkatimize majukumu yenu bila kuogopa” 
alisema Dkt. Magufuli.
Aidha,
 Mhe.  Dkt. Magufuli amesikitishwa na utafiti wa watumishi uliofanywa 
katika Mikoa ya Singida na Dodoma ambapo imegundulika watumishi 202 
wanalipwa mishahara hewa.
Wakati
 wa utafiti huo, zaidi  ya watumishi 26,900 walioko katika Halmashauri 
14 za Mikoa hiyo, watumishi 3,320 hawakuwepo kazini kwa sababu 
mbalimbali.Kwa
 mantiki hiyo, ukichukua utafiti huo wa Mikoa miwili ni dhahiri Serikali
 inapoteza mapato mengi kwa kulipa mishahara ya watumishi hewa nchi 
nzima.
Vivyo
 hivyo, Mhe. Dkt. Magufuli amewasisitiza Wakuu wote wa Mikoa wakasimamie
 ilani ya uchaguzi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwakuwa waliahidi 
kutatua kero za wananchi na wahakikishe wanazitatua ili wananchi waishi 
vizuri kwa amani ndani ya nchi yao.
Naye
 Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan amewataka Wakuu wa Mikoa na 
Wakurugenzi wa Majiji na Halmashauri zote nchini wajiandae kupokea na 
kuzipangia matumizi shilingi milioni 50 za kila Kijiji zilizoahidiwa 
wakati wa kampeni kwa lengo la kuboresha na kuimarisha shughuli za 
maendeleo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni