NAIBU WAZIRI WA MICHEZO ANASTAZIA WAMBURA ATEMBELEA KITUO CHA UTAMADUNI KIKICHOPO CHUO KIKUU CHA TUMAINI MAKUMIRA


1Wasanii wa Kituo cha Utamaduni kilichopo chuo Kikuu cha Tumaini Makumira wilaya ya Arumeru mkoani Arusha  wakicheza ngoma ya Sindimba wakati  Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura (hayupo pichani) alipotembelea kituo hicho hivi karibuni kwa ajili ya kuona shughuli za kitamaduni zinazofanyika kituoni hapo.
2Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura (wa pili kulia) akiwaangalia wasanii wa Kituo cha Utamaduni kilichopo chuo Kikuu cha Tumaini Makumira wilaya ya Arumeru mkoani Arusha (hawapo pichani)  wakicheza ngoma ya kabila la wa Meru wakati   alipotembelea kituo hicho hivi karibuni kwa ajili ya kuona shughuli za kitamaduni zinazofanyika kituoni hapo. Kulia ni Randall Stubbs ambaye ni Meneja Mradi wa kituo hicho kinachojengwa chuoni hapo, watatu kulia ni Afisa Michezo wa Mkoa Mwamvita Okeng’o na wa nne kulia ni Afisa utamaduni wilaya ya Arumeru Senyael Pallangyo.
3  5Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura akiangalia mchoro wa ramani ya  Kituo cha Utamaduni kinachojengwa katika chuo Kikuu cha Tumaini Makumira kilichopo wilaya ya Arumeru mkoani Arusha wakati alipotembelea kituo hicho hivi karibuni kwa ajili ya kuona shughuli za kitamaduni zinazofanyika kituoni hapo. Kulia ni   Afisa utamaduni wilaya ya Arumeru Senyael Pallangyo akifuatiwa  na Randall Stubbs ambaye ni Meneja Mradi wa kituo hicho.
4 Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura (watatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na wasanii wa Kituo cha Utamaduni kilichopo chuo Kikuu cha Tumaini Makumira kilichopo wilaya ya Arumeru mkoani Arusha wakati alipotembelea kituo hicho hivi karibuni kwa ajili ya kuona shughuli za kitamaduni zinazofanyika kituoni hapo.
Picha na wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni