Naibu
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. 
Hamisi Kigwangalla akitoa hotuba yake katika semina hiyo. Kushoto ni 
Mwasisi wa Taasisi ya Millen Magese, Millen Happiness Magese. (Picha na Video na Andrew Chale,Modewjiblog).
Naibu 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi
 Kigwangalla (wa kwanza kushoto) akifuatiwa na Mwanadada, Millen 
Happiness Magese (katikati) pamoja na Afisa Elimu Manispaa ya Kinondoni,
 Bw. Rogers Shemwelekwa.
Serikali
 kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, 
imesema kuwa ipo tayari kushirikiana na wadau mbalimbali akiwemo 
Mwanadada Millen Magese na Taasisi yake katika mapambano ya ugonjwa na 
athari za Endometriosis ambao unawapata wanawake wengi hapa nchini.
Kauli 
hiyo imetolewa mapema leo Machi 30.2016 na Naibu Waziri wa Afya, 
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla 
wakati wa kufungua rasmi semina maalum kwa vijana wapatao 500 wa shule 
za Sekondari zikiwemo za Turiani Sekondari,Makurumla na zinginezo za 
Manispaa ya Kinondoni pamoja na walezi na walimu, ambapo katika mkutano 
huo, Dk. Kigwangalla amebainisha kuwa, juhudi zinazofanywa na Mwanadada 
Millen Magese ni za kuungwa mkono hivyo wataendelea kushirikiana naye 
bega kwa bega.
Dk. 
Kigwangalla amebainisha kuwa, anatambua wanawake wengi duniani kote 
wanasumbuliwa na tatizo hilo ambapo gharama zake kwa kawaida ni kubwa 
huku bado wataalam wanaendelea kushughulikia namna ya upatikanaji wa 
tiba yake ili kuweza kuwa nafuu.
“Napongeza
 juhudi za dhati zinazofanywa na taasisi ya Millen Magese, katika kuunga
 mkono juhudi za serikali ya tano kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya 
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto za kuwasogeza wananchi karibu na huduma 
bora kwa ajili ya Maendeleo na Ustawi wa Jamii yetu.
Tatizo
 la kutoshika mimba (kitaalamu Endomytiosis) hutokana na sababu 
mbalimbali, nyingi zikichangiwa na uelewa mdogo wa jamii inayomzunguka 
msichana au mama anayejianadaa kuanza kubeba mimba, lakini pia upungufu 
wa vifaa tiba hospitalini na kwenye vituo vya afya sambamba na 
kukosekana kwa wataalamu katika hospitali zetu, Hivyo tunapenda kuchukua
 fursa hii kupongeza juhudi kama hizi za kuandaa semina na warsha ikiwa 
ni hatua madhubuti na ya msingi katika kuikabiliana na changamoto ya 
uelewa wa tatizo hili katika jamii.
Kwani,
 tunaamini, limekuwa jambo la faraja sana, tangu Magesse alipojitokeza 
hadharani na kuihabarisha dunia juu ya tatizo hili linalomkabili yeye 
binafsi. Naomba kusema wazi kuwa, huo ulikuwa uthubutu wa pekee wa 
mrembo huyo, kiasi cha kuifanya jamii kubwa ya kimataifa kuanza 
kulifuatilia tatizo hili ili kusaidia mabinti wadogo ambao walikuwa 
hawajakumbwa na hali hiyo. “ alieleza Naibu Waziri Dk. Kigwangalla 
katika hotuba yake hiyo.
Aidha,
 Dk. Kigwangalla aliongeza kuwa, ni faraja kubwa kwa watanzania tangu 
Magese Foundation ilipoanzishwa ikifanya kazi kubwa ya kuhamasisha 
upatikanaji wa vifaa na pia ujenzi wa hospitali maalumu kwa ajili ya 
kutibu tatizo hilo. Jambo hilo linaendelea kuitia moyo serikali hususani
 Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kufikia 
lengo la kumuwezesha mtoto wa kike kufikia malengo tarajiwa.
Kwa 
upande wake, Mwanadada Millen Magese amewaeleza vijana wa kike katika 
semina hiyo kuwa, wawe wazi pindi wajisikiapo dalili mbalimbali wakati 
wanapokuwa katika mzunguko wa siku zao ambapo na kubainisha kuwa, jambo 
hilo endapo litabainika mapema ni rahisi kulipatia tiba kuliko kuficha 
na kufika steji mbaya.
Mwanadada,
 Millen Magese pia alitumia wasaha huo kuishukuru Serikali kwa namna 
walivyokubaliana kushirikiana naye bega kwa bega katika mapambano dhidi 
ya tatizo hilo hapa nchini ambapo pia amewashukuru wadau wote kwa kuwa 
naye dhidi ya mapambano hayo.
Semina
 hiyo pia imeweza kukusanya watu mbalimbali wakiwemo watu maarufu 
wasanii, wanamitindo na wabunigu wa mavazi, wafanyabiashara na 
wanaharakati wanawake katika maendeleo hapa nchini huku wanaume nao 
wakijumuika pamoja ilikusambaza ujumbe huo kwa wenza wao na marafiki 
zao.
Tazama MO tv, kuona tukio hilo hapa:
Mwanadada, Millen Happiness Magese.
Baadhi ya wanafunzi, wadau wanaosaidiana na mwanadada Millen Magese wakifuatilia semina hiyo.
Baadhi
 ya wageni waalikwa, wakiwemo waliowahi kushiriki mashindano ya 
ulimwende hapa nchini ..wakiwa wamejumuika pamoja kuungana na taasisi ya
 Millen Magese.
Wanafunzi wakifuatilia semina hiyo.
Wanafunzi wakifuatilia semina hiyo.
Afisa Elimu Manispaa ya Kinondoni, Bw. Rogers Shemwelekwa akitoa hotuba fupi katika semina hiyo
Baadhi
 ya wadau walioungana kwa pamoja kusaidiana na taasisi ya Millen Magese 
wakifuatilia semina hiyo. Mustafa Hassanali pamoja na Rio Paul ambao 
wote ni wabunifu wa mavazi hapa nchini.
Seven Mosha na Miss Tanzania 2008, Nasreen Kareem.
Mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni, akitoa hotuba yake.
Mmoja wa madaktari bingwa wa wanawake wa Hospitali ya Muhimbili akitoa maelezo machache. 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni