KWA NINI AGIZO LA AGP MANGU LINAPUUZWA?


Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu.
Na:George Binagi @BMG
Kwa muda mrefu
kumekuwepo na malalamiko kwamba waendesha bodaboda nchini wamekuwa hawatii
sheria za usalama barabarani, hali ambayo imekuwa ikisababisha ongezeko la
ajali zinazoweza kuzuilika.
Hali hiyo ilimsukuma Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu mwishoni mwa mwezi
uliopita, kutangaza Oparesheni kamata bodaboda wasiotii sheria za usalama
barabara nchini nzima katika kikao kazi kilichowahusisha Maofisa Wakuu wa
Polisi nchini wakiwemo Makanda wa Polisi Mikoa, Vikosi na Makao Makuu, kilichofanyika
Jijini Dar es salaam.
“Pamoja na kuendelea kudhibiti uhalifu wa aina zote, natoa maelekezo kwa kila Mkoa
kuhakikisha unaendesha oparesheni kali dhidi ya bodaboda ili kupunguza ajali
zinazosababishwa na bodaboda ambao hawataki kufuata sheria na kanuni za usalama
barabarabi”. Alisema IGP Mangu na kuainisha makosa yatakayosababisha bodaboda
kukamatwa kuwa ni pamoja na Kubeba Mishikaki (abiria zaidi ya mmoja), Kutovaa
kofia ngumu (helment) pamoja na kupita katika taa za barabarani huku taa
nyekundu zikiwa zinawaka.

Soma Zaidi HAPA.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni