Kiwavijeshi aina ya Fall Armyworm (FAW).
Na Mathias Canal, Dar es salaam 
Wizara
 ya Kilimo Mifugo na Uvuvi imeanza jitihada za kuwakabili Viwavijeshi 
wapya aina ya Fall Armyworm (FAW) wanaojulikana kitaalamu kama 
Spodoptera Frugiperda ambao wametajwa kuwa na uwezo mkubwa kuharibu 
mazao mbalimbali hususan mahindi ambayo ndio zao kuu la chakula nchini.
Imeelezwa
 kuwa Viwavijeshi hao wanapofika kwenye mazao hutoa kemikali ambayo 
huweza kudanganya mmea kuwa unashambuliwa na magonjwa kama ukungu au 
fangasi hivyo mmea unapohisi unashambuliwa na hayo magonjwa, hupunguza 
kinga dhidi ya wadudu hao hatari na kuwa rahisi kushambuliwa. 
Hayo 
yamebainishwa leo Septemba 14, 2017 na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya 
Maendeleo ya Mazao kutoka Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi, Bwana Beatus
 Malema wakati akifungua warsha ya siku moja mbele ya Wadau wa Kilimo 
ambao ni Shirika la Maendeleo la Watu wa Marekani USAD, ONE HACKER FUND,
 Taasisi ya Utafiti wa Viuatilifu Ukanda wa Kitropiki  (TPRI), Shirika 
la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), na Mradi wa WEMA .
Mkurugenzi
 Msaidizi wa Idara ya Maendeleo ya Mazao Wizara ya Kilimo Mifugo na 
Uvuvi, Bwana Beatus Malema akizungumza wakati akifungua warsha ya siku 
moja kujadili namna ya kukabiliana na mdudu aina ya Kiwavijeshi.
Mkutano
 ulikuwa na lengo la kujenga uelewa wa pamoja kwa ajili ya kumkabili 
mdudu huyo aina ya Fall Armyworm (FAW) ambaye anashambulia mazao 
mbalimbali nchini hususani zao la mahindi.
Alisema
 Athari ya viwavi jeshi haishii kuharibu majani ya mimea pekee, wadudu 
hao wanapokula majani na kutengeneza sumu aina ya ‘firenide’ inayodhuru 
mifugo inapokula majani yaliyoathiriwa.
Bwana 
Malema amesema tayari Serikali imechukua juhudi za awali kukabiliana na 
mdudu huyo ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kwa wananchi juu ya utambuzi 
wa mdudu huyo kwa kuwataka Wananchi kung’oa mazao na kuyachoma pindi 
wanapobaini uwepo wa mdudu huyo.
Pia 
tayari dawa tatu zimepitishwa na Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi 
kupitia Taasisi ya uchunguzi wa Viatilifu (TPRI) zinazoangamiza wadudu 
hao ambazo ni Duduba 450, Mupacrone 500 EC na Match Save kutoka Kampuni 
ya Syngenta hivyo Wananchi wametakiwa kuzitumia haraka pindi wanapoona 
dalili za kuwepo wa wadudu hao shambani.
Wadau wa 
kilimo kutoka Shirika la Maendeleo la Watu wa Marekani Wizara ya Kilimo 
Mifugo na Uvuvi, USAD, ONE HACKER FUND, Taasisi ya Utafiti wa Viuatilifu
 Ukanda wa Kitropiki (TPRI), Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa 
Mataifa (FAO), na Mradi wa WEMA wakimsikiliza Mkurugenzi Msaidizi wa 
Idara ya Maendeleo ya Mazao Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi, Bwana 
Beatus Malema akizungumza wakati akifungua warsha ya siku moja kujadili 
namna ya kukabiliana na mdudu aina ya Kiwavijeshi.
Bwana 
Malema amesema kuwa katika kipindi cha miaka mingi Tanzania imekuwa 
ikikumbwa na viwavijeshi aina ya African Armywarms ambapo mara zote 
imekuwa ikiwadhibiti wadudu hao wanapojitokeza kwa kuwapa kiuatilifu 
kinachosababaisha matumbo ya wadudu hao kujaa na hatimaye kuwasababishia
 vifo.
Ameongeza
 kuwa kwa mara ya kwanza Wizara ilipata taarifa ya uvamizi katika shamba
 la Mwekezaji mkubwa Wilayani Nkasi Mkoani Rukwa mwezi Machi 2017 na 
walipofuatilia na kupeleka sampuli maabara mdudu huyo alibainika kwa 
jina la  Spodoptera frugiperda au Fall arymworm ambaye ni hatari na 
amekuwa akiripotiwa katika maeneo mbalimbali duniani.
Kutokana
 na unyeti wa suala hilo Wizara ya Kilimo imewasiliana na  Shirika la 
Chakula Duniani (FAO), kwa ajili ya kuunganisha juhudi za pamoja ili 
kumdhibiti mdudu huyo kabla hajasambaa kwenye maeneo mengi nchini.
Kaimu 
Mkurugenzi Msaidizi Afya ya Mimea, Idara ya Maendeleo ya Mazao katika 
Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi, Bibi Beatrice Palangyo akiwasilisha 
mada ya utambuzi wa Viwavijeshi wapya aina ya Fall Armyworm (FAW) 
wanaojulikana kitaalamu kama Spodoptera Frugiperda wakati wa warsha ya 
kujenga uelewa juu ya wadudu hao.
Shirika
 la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) katika taarifa yake 
imesema viwavijeshi hao aina ya Fall armyworm wameonekama pia katika 
nchi za Zimbabwe, Malawi, Msumbiji, Namibia Afrika ya Kusini na Zambia 
huku chanzo chake ikiwa ni nchini Marekani.
Kwa 
mujibu wa Redio ya Umoja wa Mataifa, FAO bado haijatangaza   kiwango 
kamili cha uharibifu katika nchi hizo, huku ikiongeza kuwa Shirika hilo 
na Wadau wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) 
wamejadili  udhibiti wa viwavijeshi.
Naye 
Kaimu Mkurugenzi Msaidizi Afya ya Mimea, Idara ya Maendeleo ya Mazao 
katika Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi, Bibi Beatrice Palangyo 
akiwasilisha mada ya utambuzi wa wadudu hao katika warsha hiyo amesema 
kuwa katika Nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara wadudu hawa walianza 
kuingia nchini Nigeria na kwa sasa wameenea katika nchi mbalimbali 
ikiwemo Tanzania, Afrika kusini, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo na 
Malawi.
Alisema
 wadudu hao wanashambulia mazao ya jamii ya nafaka kama mahindi (Corn) 
wanauwezo wa kushambulia hata magugu pale wanapokosa mazao kama mahindi 
kwani hawali mazao mengine kama mboga na matunda, wanakula zaidi mahindi
 na magugu yanayofanana na mahindi.
Zaidi 
ya Mikoa 15 nchini ikiwemo Zanzibar imeripoti kuwepo kwa kadhia ya mdudu
 huyo hivyo asilimia 15 ya mazao jamii ya nafaka kama mahindi 
yameathiriwa, jambo ambalo kama lisingepatiwa ufumbuzi wa haraka, 
lingesababisha upotevu mkubwa wa mazao mashambani na kutishia 
upatikanaji wa chakula nchini.


Hakuna maoni:
Chapisha Maoni