Na mwandishi wetu, Kondoa
Uingizaji
 wa mifugo kwenye pori la akiba la Mkungunero lililoko wilayani Kondoa 
mkoani Dodoma umeathiri uhifadhi wa pori hilo na kusababisha kukauka kwa
 baadhi ya vyanzo vya maji na kutoweka kwa baadhi ya wanyamapori adimu.
Meneja
 wa Pori la akiba la Mkungunero, Emmanuel Bilaso akizungumza na a 
waandishi wa habari waliotembelea pori hilo hivi karibuni amesema pori 
hilo linalopakana na Hifadhi ya Taifa ya Tarangire lina vyanzo muhimu 
vya maji ambayo yanayotegemewa na wananchi wengi kwa shughuli za kijamii
 na kiuchumi.
Bilaso
 amesema pori hilo la Mkungunero pia lina vyanzo vya maji ya mto 
Tarangire ambao ndiyo uhai wa Hifadhi ya taifa ya Tarangire na akatoa 
wito kwa wananchi kutilia mkazo uhifadhi ambao una umuhimu mkubwa kwa 
jamii na maendeleo ya taifa.
Amesema
 operesheni inayoendelea katika pori hilo imefanikisha kukamata kwa 
mifugo mingi katika pori hilo ambayo inachunga humo kinyume na sheria ya
 uhifadhi ambayo inakataza shughuli za binadamu kwenye maeneo 
yaliyohifadhiwa.
“Tumekamata
 ng’ombe zaidi ya 230 ambao waliingizwa na wananchi kinyume cha sheria 
na wamefikishwa mahakamani na kutozwa faini ya zaidi ya shilingi milioni
 6” alisema bwana Bilaso.
Aliongeza
 kuwa kuingiza ng’ombe ndani ya hifadhi ni kinyume cha sheria ya 
uhifadhi ambayo inatoa adhabu kali ikiwemo kutaifisha mifugo 
inayokamatwa ili iwe fundisho kwa watu wanaovunja sheria za uhifadhi.
Nae
 Mkuu wa mkoa wilaya ya Kondoa Sezaria Makota amewaonya wananchi 
wanaingiza mifugo katika pori hilo kuacha mara moja vinginevyo hatua 
kali zitachukuliwa dhidi yao ili iwe fundisho kwa watu wanaovunja sheria
 na kuingiza mifugo kwenye maeneo yaliyohifadhiwa.
Amesema
  wilaya inaandaa mkakati wa uwepo wa makao makuu ya ncho Dodoma na 
kukamilika kwa ujenzi wa barabara ya lami kutoka Dodoma mpaka Babati 
kuwa fursa ya kiuchumi kwa wananchi na taifa.
“Tuna
 vivutio vingi vya utalii likiwemo pori la akiba la Mkungunero na 
mapango yenye michoro ya kale, ni matarajio yetu kwamba viongozi wengi 
na wabunge watapata fursa ya kutembelea na hasa kwa sasa ambapo barabara
 ya lami kutoka Dodoma mpaka Babati imekamilika´alisema mkuu wa wilaya.
lenye
 wanyamapori wengi wakiwemo simba, tembo, nyati na mimea adimu meneja wa
 pori la akiba la mkungunero emmanuel bilaso amesema watuhumiwa 
waliokamatwa
Nao
 baadhi ya wananchi wanaoishi kwenye vijiji kuzunguka pori hilo 
wameiomba serikali kuweka vipaumbele katika uhifadhi wa pori hilo la 
akiba la Mkungunero ikiwemo kulipa fidia kwa baadhi ya wananchi 
wanaotakiwa kupisha uhifadhi endelevu wa pori kama tathimini 
ilivyofanywa na serikali kwa mujibu wa sheria.
Diwani
 wa kata ya Itaswi  Said Mohamed Chobu alisema wananchi wanatambua 
umuhimu wa pori hilo lakini ni vizuri sasa wizara ya maliasili na utalii
 ikalipa fidia kwa wananchi kwenye vijiji kandokando ya hifadhi ili 
kuepuka uharibifu wa mazingira na migogoro baina ya wananchi na 
wahifadhi.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni