RC SHIGELLA:WANAWAKE WANA MCHANGO MKUBWA KWA JAMII


Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella kushoto akilakiwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa wakati alipokwenda kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya wanawake dunia ambapo kimkoa ilifanyika kwenye viwanja vya Kange jijini Tanga
 Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella kushoto akiwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa wakati alipokwenda kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya wanawake dunia ambapo kimkoa ilifanyika kwenye viwanja vya Kange jijini Tanga 
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella akisalimia na Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga (DAS) Faidha Salim wakati alipokwenda kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya wanawake dunia ambapo kimkoa ilifanyika kwenye viwanja vya Kange jijini Tanga 
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella kushoto akilakiwa na kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Tanga mara baada ya kuwasilia kwenye viwanja hivyo wakati alipokwenda kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya wanawake dunia ambapo kimkoa ilifanyika kwenye viwanja vya Kange jijini Tanga kulia ni mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa anayefuata ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga (Ras) Mhandisi Zena Saidi
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella akisalimiana na watumishi mbalimbali wakati alipokwenda kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya wanawake dunia ambapo kimkoa ilifanyika kwenye viwanja vya Kange jijini Tanga
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella akisalimiana na Afisa Matekelezo wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya afya Mkoani Tanga (NHIF) Macrina Clemens wakati alipokwenda kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya wanawake dunia ambapo kimkoa ilifanyika kwenye viwanja vya Kange jijini Tanga
Sehemu ya wanawake wakiwa kwenye maandamano wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambapo kimkoa ilifanyika kwenye viwanja vya Kange Jijini Tanga
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella katika akipokea maandamano ya wanawake wakati wa maadhimisho ya siku yao kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Mhandisi Zena Saidi kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella kushoto akipata maelezo kutoka kwa maafisa wa benki ya Amana wakati alipotembelea banda lao kwenye maadhimisho hayo wa kwanza kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga (Ras) Mhandisi Zena Saidi
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella kushoto akipata maelezo kutoka kwa maafisa wa benki ya Amana wakati alipotembelea banda lao kwenye maadhimisho hayo wa kwanza kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga (Ras) Mhandisi Zena Saidi
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella akiwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Saidi wakiangalia bidhaa zinazozalishwa na wajasiriamali wanawake
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella kulia akifuatilia matukio mbalimbali kwenye maadhimisho hayo kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga (RAS) Mhandisi Zena Saidi na anayefuatia ni Diwani wa Kata ya Maweni(CCM) Calvas Joseph
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella akizungumza wakati wa maadhimisho hayo
Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa akizungumza katika maadhimisho hayo
Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga,Faidha Salim katika akishiriki kuimba wimbo na wakina mama wa ngomba ya msanja wakati wa maadhimisho hayo
Diwani wa Viti Maalumu (CCM) Kata ya Chumbageni Saida Gadafi akimtunza msaanii aliyekuwa akitumbuiza kwenye maadhimisho hayo
Sehemu ya wanawake kutoka Taasisi ya BRAC wakifuatilia maadhimisho hayo

NA MWANDISHI WETU,TANGA.

MKUU wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella amesema wanawake wana mchango mkubwa kwa jamii hivyo wanapaswa kuheshimiwa na kupewa kipaumbele ili waweza kupata mafanikio.

Aliyasema hayo wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambapoalisema lazima jamii iwaheshimu wanawake na kuwapa nafasi ili wawezekutimiza ndoto zao kwani wao ndio kila kitu.

Alisema wanawake ndio nguzo kubwa ya kuweza kusaidia chachu ya maendeleo kwa jamii hivyo lazima wapewe nafasi ya kuchangamkia fursa zilizopo.

"Tuna uhakika na mama zetu waliotuzaa,kutulea na kutunyonyesha lakainihatuna uhakika na Baba zetu maana wao hivyo lazima tuwaheshimu nakuwapa kipeumbele kwa kila jambo "Alisema.

Alisema mwanamke ni kila kitu katika maisha hivyo wanastahili kupewapongeza kutokana na namna wanavyosaidia kuilea jamii na hatimaye kuwezakutimiza malengo yao.

"Sisi duniani kote tuna uhakika na mama zetu maana wao ndio waliotuzaa nakutulea na kunyonyesha lakini hatuna uhakika na baba zetu hivyo lazimatuwaheshima na kuwajali maana ndio wametufikishaa hapa mwanamke ndio kila kitu ni mama, dada, shangazi,bibi na my sweet darling Alisema RC Shigella.

Hata hivyo alisema ni vema wanawake waheshimiwe na ndio maana serikali yaawamu ya tano chini ya Rais Dkt John Magufuli anawapenda na kuwathaminina ndio maana akamteuwa Makamu wa Rais Samia Suluhu katika nafasi ya juu kumsaidia.

"Hivyo hii inaonyesha namna anavyowathamini na kutambua mchango wenukwenye kuchochea kasi ya ukuaji waa maendeleo"Alisema

Alisema tuna wajibu wa kuhakikisha tunaenzi jitihada za Rais wetu kwa kuthamini wanawake na kuwapa nafasi ili waweze kutimiza malengo yao waliojiwekea kufikia.

Mkuu huyo wa mkoa alisema jamii inawajibu wa kuwawezesha wanawake kupitia Taasisi mbalimbali kwa kuwapa nafasi za uongozi kwenye viwanda vilivyopo mkoani Tanga kwa kuzingatia jinsia na usawa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni