Mawasiliano ya simu kuvifikia Vijiji vyote nchini kwa gharama nafuu


Serikali kwa kushirikiana na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote imejipanga kuhakikisha vijiji vyote nchinivinapata huduma ya Mawasiliano ya simu za Mkononi kwa gharama Nafuu ifikapo mwakanin,2019.

Akiongea na waandishi wa habari jijini Arusha  katika mkutano wa siku mbili wa Taasisi za udhibiti waMawasiliano katika nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki(EACO),Naibu waziri wa Uchukuzi na MawasilianoMhandisi Atashasta Nditie.

Amesema hadi sasa Tanzania ina asilimia 94 ya wananchi  wanaotumia mawasiliano ya Simu za Mkononina kwamba ifikapo mwaka 2019 watanzania wote watafikiwa na huduma hiyo ya mawasiliano ya uhakika .

''Ndani ya kipindi cha mwaka mmoja watanzania wote watakuwa wamefikiwa na mawasiliano ya uhakika naNinaposema mawasiliano simaanishi Mitandao yote ya Simu iwafikie ila tunamaanisha hata mtandaommoja ukifika tayari watanzania watakuwa wamefikiwa na mfumo wa Mawasiliano "Amesema Naibu waziri

Katika hatua nyingine Mhandisi Nditie Amesema mfuko wa mawasiliano kwa wote utajenga Minara yamawasiliano kwa vijiji 369 kuanzia mwezi ujao wa kumi ,hivyo kuongeza huduma ya mawasiliano,jambolitakalosaidia kuimarisha uchumi kupitia sekta ya mawasiliano.

Awali  katibu Mtendaji wa  taasisi  ya mawasiliano ya Afrika Mashariki (EACO),Ally Simba amesema.nchi zajumuia ya Afrika Mashariki zimepiga hatua kubwa katika mawasiliano ya Simu za Mkononi kwa asilimia 50na Intaneti asilimia75 ikiwemo  Tanzania yenye asilimia 94,Kenya asilimia 90 na Uganda ni asilimia 70.

Lengo la mkutano huo ni kuhakikisha vijiji vyote vilivyoko katika nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki visivyona Mawasiliano vinapata huduma hiyo  "Amesema

Naye Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano NchiniTCRA),Mhandisi James  Kilaba Amesema Mamlakahiyo itaendelea kudhibiti maudhui ya mawasiliano  pamoja na kusimamia  sheria ya mtandaoni

"Tanzania imekuwa nchi ya kwanza kwa nchi za jumuiya ya Afrika mashariki kwa kuanzisha mfuko maalamukwa ajili ya kupeleka huduma ya mawasiliano kwenye vijiji ambavyo kampuni za Simu zinaona havina mvutowa kibiasharaAmesema

Amesema mamlaka ya mawasiliano nchini imelazimika kuuza kwa mnada Masafa ya mwendo kasi ilikuwawezesha wananchi kote nchini kupata huduma ya Mawasiliano ya uhakika.
 
Mkurugenzi wa TCRA James Kilaba

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni