Shule ya msingi Sing’isi iliyopo katika wilaya ya Arumeru Mkoani 
Arusha iliyokuwa ikikabiliwa  na changamoto ya madarasa kujaa maji 
imepatiwa msaada wa kiasi cha shilingi Milioni nne na benki ya biashara 
ya Africa (CBA) kwa ajili ya ukarabati wa baadhi ya madarasa
Akikabidhi
 hundi katika shule hiyo juzi Mkurugenzi wa CBA Gifti Shoko alisema kuwa
 lengo la msaada huo ni kusaidia wanafunzi kuondokana na changamoto ya 
kutoa maji katika madarasa pindi mvua zinaponyesha hali inayosababisha 
kukosa vipindi viwili hadi vitatu kwa siku
Alisema
 kuwa msaada huo utumike kama ulivyokusudiwa kuboresha madarasa hayo 
kwani ubora wa elimu unaletwa na mazingira mazuri ya watoto  kusomea  
‘’Hapa
 nawaona Marais, mawaziri wa kesho pamoja na wafanyakazi wazuri wa benki
 yetu hivyo hatuna budi kutuoa msaada huu ikiwa kama mchango wetu wa 
kuboresha sekta ya elimu na tunawahidi hatutaishia hapa tutaendelea 
kuwasaidia kadri ya uwezo wetu ‘’
Mwalimu
 mkuu wa shule hiyo Faith Mushiro akitoa neno la shukrani alisema kuwa 
wanafunzi wa darasa la tano na la sita ndiyo hasa walikuwa wakipata 
hadha hiyo ya kuondoa maji madarasani pindi mvua zinapoanza kunyesha
Aidha
 alisema kuwa zaidi ya vipindi viwili hadi vitatu vya asubuhi hushindwa 
kuhudhulia kutokana na changamoto hiyo hivyo kupitia msaada huo 
wanafunzi watasoma katika vyumba  vya madarasa vizuri tofauti na kipindi
 cha nyuma 
Awali
 akisoma Risala mwalimu wa shule hiyo Bw.Simon Mbawala  kwa niaba ya 
shule hiyo alisema kuwa pamoja na msaada waliopatiwa bado shule 
inakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa makataba ya kuhifadhi vitabu, 
kuharibika kwa sakafu za madarasa pamoja na kupasuka kwa vioo vya 
madirisha 
Hata
 hivyo tunatoa shukrani zetu za dhati kwa mssada huu wa ujenzi wa vyumba
 vinne ambayo vilikuwa na tatizo la kuvuja kwa maji kutokana na bati 
zake kuwa chakavu hali iliyokuwa ikiwathiri sana wanafunzi na walimu 
hasa ikifika wakati wa kufundisha
 Mkurugenzi
 wa Benki ya biashara ya Africa (CBA) Gifti Shoko akikabidhi hundi ya 
kiasi cha shilingi Milioni nne kwa Mwalimu mkuu wa Shule ya msingi 
Sing’isi iliyopo katika wilaya ya Arumeru Mkoani Arusha juzi Bi.Faith 
Mushiro kwaajili ya kukarabati madarasa manne ambayo hujaa maji kipindi 
cha mvua hali ambayoilikuwa ikiwasababishia wanafunzi kukosa vipindi 
viwili hadi vitatu kwa siku.
 Mwalimu
 Mkuu wa Shule ya Msingi Sing'isi Bi.Faith Mushiro akionyesha sehemu 
ambayo husababisha maji kujaa ndani ya madarasa pindi mvua inaponyesha, 
wakatikati ni Mkurugenzi wa Benki ya biashara ya Africa(CBA)Gifti Shoko 
pamoja na wafanyakazi wa benki hiyo
 Mwalimu
 Mkuu wa shule ya msingi  Sing'isi Bi.Faith Mushiro akitoa neno la 
shukrani kwa uongozi wa benki ya CBA mara baada ya kupata msaada wa 
shilingi Millioni nne kwa ajili ya ukarabati wa madarasa.
 Mkurugenzi
 wa Benki ya biashara ya Africa(CBA)Gifti Shoko akiangalia baadhi ya 
vifaa vya umeme ambavyo walitoa msaada kwa shule hiyo
 Wanafunzi wakiimba
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni