WANANCHI WA KOREA KUSINI WAPIGA KURA KUMCHAGUA RAIS WAO

Wananchi wa Korea Kusini wanapiga kura kumchangua rais, katika uchaguzi ulioitishwa baada ya rais kuondolewa madarakani kutokana na kashfa kubwa ya rushwa.

Mgombea mliberari Moon Jae-in anaelekea wazi kuongoza kwa kura huku akichuana na Ahn Cheol-soo wa siasa za mrengo wa kati.

Uchaguzi huo unafuatiliwa kwa karibu na dunia wakati huu wa hali tete ya uchumi na hofu ya kutokea vita na Korea Kaskazini.
Mgombe Moon anataka kuongeza uhusiano na Korea Kaskazini, kinyume na kiongozi aliyeondolewa Park Geun-hye aliyekata mahusiano yote na jirani zao hao.
  Wananchi wa Korea Kusini wakitimiza haki yao ya Kikatiba ya kupiga kura kumchagua rais

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni