WATU WAWILI WAMEUWAWA MMOJA KATIKA AJALI NA WAPILI KUPIGWA HADI KUFA WILAYANI KONDOA DC

Image result for haubi kondoa

Na Mahmoud Ahmad Kondoa
Watu wawili ambao hawajatambuliwa majina yao hadi sasa wanaokiwa kuwa na umri tofauti kati ya miaka 37 hadi 40 mmoja dereva wa Katapila lenye no za usajili T 370 BBG lililokuwa likitengeneza barabara ya Haubi na kumgonga mtu mmoja hadi kufa na wananchi wenye hasira kumpiga dereva huyo hadi kumuua.
Tukio hilo limetokea wilayani Kondoa dc Kata ya Haubi kijiji cha haubi baada ya dereva huyo ambaye jina lake halijapatikana hadi sasa kumgonga mwenda kwa miguu na kusababisha kifo chake hapo hapo.
Mmoja wa mashuhuda aliekuwepo eneo la tukio Mohammed Kijaji alisema kuwa tukio hilo lilitokea majira ya saa 12;45 jioni ya tarehe 13 mwezi huu baada ya mwenda kwa miguu huyo ambaye hakutambuliwa jina kuwa anatembea pembezoni mwa barabara na ndipo katapila hilo kumgonga na kufa hapo hapo.
Kijaji alisema kuwa wananchi wenye hasira kali ndipo walimvamia mwananchi huyo na kumpiga hadi kufa dereva huyo na kusababisha mauti yake papo hapo na baada ya kumuuwa waliendelea kuleta fujo hadi polisi walipofika eneo la tukio na wananchi hao kutawanyika.
Kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma Lazaro Mambosasa alithibitisha kutokea kwa tukio hilo la kuuwawa kwa watu wawili mmoja kwa ajali na mwingine kwa kupigwa na wananchi hadi kufa na jeshi la polisi linawashikilia watu wawili kwa mauuaji ya dereva huyo
Kamanda Mambosasa akizungumza kwa njia ya simu alitoa wito kwa wananchi kuacha kujichukulia sheria mikononi na jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo ambapo maiti za marehemu hao zikihifadhiwa chumba cha maiti hospitali ya wilaya ya Kondoa.
Mwisho................................................................

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni