Hussein Makame, NEC 
Tume
 ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetoa wito kwa wananchi walioko kwenye 
halmashauri mbalimbali nchini, kuitumia vyema fursa ya utoaji wa elimu 
ya mpiga kura kupitia redio za kijamii kwenye halmashauri zao ili 
kuondoa manung’uniko kwenye chaguzi.
Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume hiyo Bw. Kailima Ramadhani wakati akizungumzia mpango wa kutoa elimu ya mpiga kura nchi nzima ulioanza kutekelezwa Mei 8 mwaka huu hii katika mikoa kumi nchini.
Alisema
 kupitia mpango huo wananchi wanaosikiliza redio za kijamii kwenye 
halmashauri nchini, watapata fursa ya kujifunza elimu ya mpiga kura na 
kuelewa masuala yote muhimu yanayohusu mfumo mzima wa kupiga kura. 
“Tumepanga
 mpango, Tume itasambaa nchi nzima kuzungumzia elimu ya mpiga kura 
kwenye redio za kijamii zilizoko kwenye halmashauri zote za Jamhuri ya 
Muungano wa Tanzania.” alisema Bw. Kailima.
Alisisitiza
 kwa kutoa wito kwa wananchi walioko maeneo ambayo Tume itakwenda kutoa 
elimu ya mpiga kura, wasikilize na kuuliza maswali ili waweze kuelewa.
“Hii
 ni fursa kwa wananchi ambayo muda mrefu hawajawahi kuipata, hivyo 
nawaomba wafuatilie ili waweze kuelimika zaidi ili yale manung’uniko ya 
kura yatakuwa yamekwisha na tutakuwa na uchaguzi mzuri zaidi ya ile 
ambayo tumeifanya.” Alifafanua Bw. Kailima.
Utekelezaji
 wa mpango huo umegawanyika katika makundi matatu ambapo kundi la kwanza
 limeanza kutoa elimu hiyo elimu hiyo kwenye mikoa ya Kagera,Mwanza, 
Kilimanjaro, Morogoro, Mbeya na Dodoma.
Mikoa
 mingine itakayojumuishwa kwenye kundi hilo ni Ruvuma, Mara, Pwani na 
Mtwara ambapo elimu hiyo itatolewa kuanzia tarehe 8 Mei hadi tarehe 20 
Mei mwaka 2017.
Kundi
 la pili linatarajiwa kutoa elimu hiyo kuanzia tarehe 24 Mei hadi tarehe
 7 Juni mwaka huu katika mikoa ya Geita, Tanga, Singida, Shinyanga, 
Lindi, Arusha, Tabora, Kigoma, Iringa, Manyara, Rukwa, Katavi, Songwe, 
Njombe na Simiyu.
Bw.
 Kailima alisema kuwa utoaji wa elimu hiyo utajikita kwenye mada kuu ya 
Elimu ya Mpiga Kura iliyogawanywa kwenye vipindi vitano, itakaytoolewa 
kwenye redio hizo kulingana mada husika na wananchi kuuliza maswali na 
kujibiwa na wawasilishaji wa mada hizo kutoka Tume.
“Ni
 mada ambayo imejumuisha masuala yote muhumu yatakayofanya mpiga kura 
yeyote au mdau yeyote wa uchaguzi kuisoma au kuisikiliza na akaelewa 
mfumo mzima wa masuala ya kupiga kura” alisema.
Mbali
 na kutoa elimu ya mpiga kura kupitia vituo vya redio za kijamii katika 
halmashauri nchi nzima, Tume pia inatoa elimu hiyo kwa njia ya magazeti 
na vyombo vingine vya habari na mitandao ya kijamii, kushiriki kwenye 
mikutano na maonesho mbalimbali nchini.
Mkurugenzi
 wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Bw. Kailima Ramadhani 
akitoa elimu ya mpiga kura kupitia redio A FM ya mkoani Dodoma leo Mei 9
 mwaka huu huku akifuatiliwa kwa makini na watangazaji wa redio hiyo.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni