VYOMBO VYA HABARI KENYA KUENDESHA MIDAHALO MITATU YA WAGOMBEA URAIS

Vyombo vya habari nchini Kenya vitaendesha midahalo mitatu ya wagombea urais mwezi mmoja kabla ya Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Agosti mwaka huu.

Midahalo hiyo ya urais itafanyika katika tarehe tofauti mwezi Julai, huku mdahalo wa kwanza wa marais ukipangwa kufanyika Julai 10.

Mdahalo wa wagombea mwenza utafuatia Julai 17 na kisha mdahalo wa mwisho wa wagombea urais Kenya kufanyika Julai 24.
Midahalo hiyo yote itafanyika kwenye chuo cha Catholic University of Eastern Africa saa moja na nusu usiku na kurushwa kwenye runinga na redioni.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni