Kijana  Frank Japhet (23), mkazi wa Mbezi, Dar es Salaam, amelazimika 
kujisalimisha katika Kituo cha Polisi Mlandizi, Kibaha, Pwani, baada ya 
mzigo wa mahindi unaokadiriwa kuwa na uzito wa kilogramu 20, anaodaiwa 
kuuiba kung’ang’ania mabegani.
Wakati akihojiwa kituoni hapo, mtuhumuwa huyo amesema mzigo huo, 
uliofungwa kwenye kiroba aliuiba kwa mama mmoja eneo la Mtaa wa 
Nyambwiro, Mlandizi, Kibaha, mkoani Pwani majira ya saa 7.00 usiku wa 
kuamkia leo Mei 3, 2018, akaongeza kwamba aliondoka na mzigo huo hadi 
eneo la Stendi ya Mlandizi alipokuwa auache kwa mwenzake ili arudie 
mzigo mwingine, ambapo mzigo huo uling’ang’ania kichwani.
Ameendelea kusema kwamba alijitahidi kufanya kila aliloweza ili mzigo 
huo utoke kichwani ikiwa ni pamoja na kulala ili akinyanyuka ubaki chini
 lakini aliponyanyuka, alinyanyuka nao kichwani! Baada ya kuzunguka nao 
kwa muda mrefu, alidai alichoka hivyo akalazimika kujisalimisha polisi 
ili asije akauawa na raia wenye hasira watakapobaini kuwa ni mwizi.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani Jonathan Shanna  amesema walilazimika 
kumtafuta mhusika wa mzigo huo ili kuweza kumsaidia kijana Frank Joseph 
ambaye aliiba kiroba hicho, baada ya wao kushindwa kumtua.
Kamanda Shanna ameendelea kusimulia kuwa wakati wakijaribu kumtua kijana
 huyo kiroba cha mahindi alichoiba alikuwa akilalamika kupata maumivu 
makali, na ndipo wakamsaka mmiliki wa mzigo ili kumsaidia.  



Hakuna maoni:
Chapisha Maoni