Katibu
 Tawala Mkoa wa Shinyanga Albert Msovela amefungua mafunzo kwa wajumbe 
wa kamati ya kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto mkoa wa 
Shinyanga yanayolenga kuwajengea uwezo wa namna ya kupiga vita ukatili 
katika jamii.
Mafunzo
 hayo ya siku tatu yaliyoanza leo Jumatano Mei 30,2018 yanayofanyika 
katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Shinyanga 
yamekutanisha wadau mbalimbali wanaohusika katika kutokomeza ukatili 
dhidi ya wanawake na watoto kwa ufadhili wa shirika lisilo la kiserikali
 la Investing in Children and their Societies (ICS – Africa). 
Awali 
akizungumza,Afisa Maendeleo ya Jamii mkoa wa Shinyanga Glory Mbia 
alisema lengo la mafunzo hayo ni kupata maoni na mapendekezo mbalimbali 
katika kutokomeza vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto. “Lengo
 la mafunzo haya ni kupata uelewa wa pamoja na kutengeneza mkakati namna
 gani tunafanya katika kutokomeza vitendo vya kikatili katika 
mkoa”,alisema Mbia. 
Akifungua
 mafunzo hayo, Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Albert Msovela ambaye ni 
mwenyekiti wa kamati hiyo alisema mkoa wa Shinyanga bado una tatizo 
kubwa la ukatili dhidi ya watoto na wanawake hivyo zinahitajika nguvu za
 pamoja 
“Tunamshukuru
 mwenyezi Mungu mauaji dhidi ya albino yamebaki historia katika mkoa 
wetu,lakini katika jamii kumekuwa na unyanyasaji hasa wa watoto,kupitia 
kamati hii naamini kwa pamoja kama tutaamua kwenda pamoja hatua kwa 
hatua tutaweza kutokomeza vitendo vya ukatili katika mkoa huu”,alieleza 
Msovela. “Akina mama na watoto wengi wameathirika 
kisaikolojia,kimwili,wapo watoto wamekosa elimu kutokana na unyanyasaji 
wanaopitia kwa pamoja naamini sheria ambazo zipo na umoja huu tutaweza 
kukabiliana na ukatili wanaofanyiwa wanawake na watoto”,alisema. 
“Kwa 
namna ya pekee niwashukuru sana wadau wetu wa maendeleo ICS ambao 
wamejitolea kudhamini mafunzo haya,na hivi sasa kamati imeshaundwa 
kutoka katika ngazi ya kata,halmashauri na sasa tunaendelea na mafunzo 
kwa ngazi ya mkoa”,aliongeza Msovela. 
Kwa 
upande wake,Afisa Maendeleo Mwandamizi, Wizara ya Afya,Maendeleo ya 
Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, Mathias Haule alisema umaskini umekuwa 
chanzo cha vitendo ukatili dhidi ya wanawake hivyo ili kutokomeza 
vitendo hivyo ni vyema wanawake wanapaswa kuwezeshwa kiuchumi huku wadau
 wote wakiweka nguvu pamoja katika kuwalinda na kuwatetea wanawake na 
watoto. 
Naye 
Meneja wa shirika la ICS nchini,Kudely Sokoine Joram alisema ili 
kutokomeza vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto,shirika hilo 
limekuwa likishirikiana na serikali ili kuhakikisha wanawake na watoto 
wanakuwa salama katika jamii. 
“Kupitia
 mradi wetu wa masuala ya ulinzi na usalama wa watoto tunafanya mradi 
huu katika manispaa ya Shinyanga,Shinyanga Vijijini na wilaya ya Kishapu
 na baada ya serikali kumaliza kutengeneza mwongozo,ilituomba tunapokuwa
 na rasilimali basi tuweze kusaidia serikali kuhakikisha kamati 
zinaundwa na zinapata mafunzo ndiyo maana hata haya mafunzo 
tumeyawezesha sisi”,alieleza. 
Meneja
 huyo wa ICS alisema katika ngazi ya halmashauri,kata na vijiji mpaka 
sasa wamezisaidia kamati 25 wakishirikiana na serikali na wanaendelea 
kuwezesha uundwaji wa kamati ili kupunguza vitendo vya ukatili dhidi ya 
wanawake na watoto. 
“Sisi 
kama wadau wa maendeleo tunashughulika na masuala ya malezi na matunzo 
bora ya watoto,masuala ya ulinzi wa watoto kwa mfano miongozo ya 
serikali na sheria zilizopo lakini pia kuwezesha familia katika masuala 
ya kiuchumi,kujenga uwezo wa taasisi ndogo ndogo na maeneo husika 
yanayoshughulika na maendeleo ya jamii”,alisema Joram. 
Katibu
 Tawala Mkoa wa Shinyanga Albert Msovela akifungua mafunzo ya kujengea 
uwezo kwa wajumbe wa kamati ya kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na 
watoto mkoa wa Shinyanga leo Mei 30,2018 - Picha zote na Kadama Malunde -
 Malunde1 blog
Katibu
 Tawala Mkoa wa Shinyanga Albert Msovela akifungua mafunzo na kuwataka 
wajumbe wa kamati hiyo kushirikiana katika kupiga vita vitendo vya 
ukatili dhidi ya wanawake na watoto mkoani Shinyanga.
Washiriki wa mafunzo hayo wakiwa ukumbini.
Afisa 
Maendeleo ya Jamii mkoa wa Shinyanga Glory Mbia akielezea malengo ya 
mafunzo hayo ambapo alisema lengoni kupata maoni na mapendekezo 
mbalimbali kuhusu namna ya kukomesha vitendo vya ukatili dhidi ya 
wanawake na watoto mkoani Shinyanga. 
Washiriki wa mafunzo hayo wakiwa ukumbini.
Meneja
 wa shirika la ICS nchini Tanzania, Kudely Sokoine Joram akizungumza 
wakati wa mafunzo hayo ambapo alisema wameamua kufadhili mafunzo hayo 
ili kushirikiana na serikali katika kutokomeza vitendo vya ukatili dhidi
 ya wanawake na watoto.
Meneja wa shirika la ICS nchini Tanzania, Kudely Sokoine Joram akizungumza ukumbini.
Kamanda
 wa polisi mkoa wa Shinyanga,ACP Simon akielezea namna wanavyoshiriki 
katika mapambano dhidi ya vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na 
watoto mkoani Shinyanga.
Washiriki wa mafunzo hayo wakiwa ukumbini.
Afisa 
Maendeleo Mwandamizi, Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na
 Watoto, Mathias Haule akielezea Muhtasari kuhusu Mpango kazi wa taifa 
wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto.
Washiriki wa mafunzo wakifuatilia mada ukumbini.
Mafunzo yanaendelea.
Kushoto
 ni Afisa Maendeleo Mwandamizi, Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, 
Jinsia,Wazee na Watoto, Mathias Haule na Afisa Mradi wa kutokomeza 
ukatili dhidi ya watoto kutoka shirika la ICS mkoa wa Shinyanga,Shadia 
Nurdin wakiangalia nyaraka zinahusu masuala ya kuzuia ukatili dhidi ya 
wanawake na watoto.Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni