Waziri
 wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiwaongoza Maafisa wa 
Wanyamapori 87 wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania– TAWA, 
Shirika la Hifadhi za Taifa – TANAPA na Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la 
Ngorongoro kupiga gwaride la ukakamavu muda mfupi baada ya kuwatunuku 
vyeti vya kuhitimu mafunzo ya Jeshi Usu hivi karibuni katika kituo cha 
Mlele mkoani Katavi.
........................................................
Wakati
 huu tunapoadhimisha miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, ni 
takriban miaka miwili sasa na miezi kadhaa tangu Serikali ya awamu ya 
tano, inayoongozwa na Mhe. Rais, Dk. John Pombe Joseph Magufuli iingie 
madarakani.
Itakumbukwa
 kuwa katika hotuba yake ya kwanza ya kulihutubia Bunge la Jamhuri ya 
Muungano wa Tanzania akiwa mjini Dodoma, Mhe. Rais Magufuli alitoa 
vipaombele kadhaa vya kutekelezwa na wizara zake huku Wizara ya 
Maliasili na Utalii akiipa vipaombele vikuu vitatu ambavyo ni 
kukabiliana na ujangili, kutatua migogoro ya mipaka kwenye maeneo ya 
hifadhi na kuongeza ukusanyaji wa mapato ya Serikali.
Wizara
 ya Maliasili imeendelea kutekeleza vipaombele hivyo pamoja na jukumu 
lake la msingi la kuhifadhi na kusimamia matumizi endelevu ya rasilimali
 za maliasili na malikale, na kuendeleza Utalii kwa faida ya kizazi cha 
sasa na kizazi kijacho.
Ujangili
Wizara
 imefanikiwa kuanzisha mikakati mbalimbali ya kukabiliana na ujangili na
 biashara haramu ya wanyamapori ambayo imeanza kuzaa matunda.
Mikakati
 hiyo ni pamoja na kuanzishwa kwa Kikosi Kazi Maalum cha Kudhibiti 
Uhalifu wa Misitu na Wanyamapori nchini ambacho kilianzishwa mwezi 
Julai, 2016 sambamba na kuimarishwa kwa Mamlaka ya Usimamizi wa 
Wanyamapori Tanzania (TAWA) ambayo ilianza majukumu yake rasmi tarehe 1 
Julai, 2016.
Mikakati
 mingine ni mabadiliko ya mfumo wa utendaji kutoka ule wa kiraia kwenda 
wa Jeshi Usu, matumizi ya teknolojia ya ndege zisizokuwa na rubani 
(drones) kwa ajili ya doria, ushirikishwaji wa wananchi kwenye uhifadhi 
na matumizi ya mbwa maalum wa kunusa ili kutambua nyara katika viwanja 
vya ndege na bandari.
Kupitia
 mikakati hiyo, mwaka 2016/2017 Wizara kupitia taasisi zake iliendesha 
doria mbalimbali ndani na nje ya maeneo yaliyohifadhiwa na kufanikiwa 
kukamata watuhumiwa 7,085 kwa makosa mbalimbali. Aidha, meno ya tembo 
129 na vipande 95 vyenye uzito wa jumla ya kilo 810.03 vilikamatwa.
Vielelezo
 kadhaa pia vilikamatwa ikiwemo silaha za kivita 48, silaha za kiraia 
150, risasi 1,058, magobore 406, silaha za jadi 22,307 na roda 120,538.
Jumla
 ya kesi 2,097 zilifunguliwa katika mahakama mbalimbali na kesi 802 
zilimalizika. Watuhumiwa 472 katika kesi 262 walifungwa jela jumla ya 
miezi 42,153 na watuhumiwa 79 katika kesi 43 waliachiwa huru huku 
watuhumiwa wengine 469 katika kesi 276 wakilipa faini ya jumla ya 
shilingi  milioni 452.1.
Katika
 kuelekea kwenye Mfumo wa Jeshi Usu, Wizara imeendesha mafunzo kwa 
watumishi 661 kuhusu ukakamavu, uongozi na ukusanyaji wa taarifa za 
kiintelijensia kuhusu Ujangili. Watumishi walioshiriki mafunzo hayo ni 
139 kutoka TAWA, 388 kutoka TANAPA, 117 kutoka Mamlaka ya Hifadhi ya 
Eneo la Ngorongoro na 17 kutoka Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania. 
Kutokana
 na jitihada hizi hali ya ujangili imepungua kwa kiasi kikubwa. Kwa 
mfano, katika Pori la Akiba Selous idadi ya Tembo waliouwawa imepungua 
kutoka tembo 17 mwaka 2015/16 hadi tembo 7 mwaka 2016/17.
Hata
 hivyo, katika siku za hivi karibuni, wanyamapori hasa tembo wameanza 
kuonekana katika maeneo mbalimbali ambayo kwa kipindi kirefu hawakuwa 
wakionekana, mfano hivi karibuni tembo kadhaa walionekana katika Chuo 
Kikuu cha Dodoma (UDOM).
Aprili
 18 mwaka huu, Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla 
akizungumza na Balozi wa Uingereza hapa nchini, Sarah Cooke ofisini 
kwake mjini Dodoma, alinukuliwa akisema kuwa ujangili hapa nchini 
umepungua kwa zaidi ya asilimia 50.
Alisema
 katika kipindi cha miezi sita iliyopita hadi kufikia mwezi huu wa 
Aprili hakuna mauaji mapya ya wanyamapori yaliyoripotiwa kuhusiana na 
ujangili na kwamba nyara zinazokamatwa hivi sasa ni masalia ya zamani 
ambayo yanatafutiwa masoko. 
Alisema
 mafanikio hayo yametokana na juhudi mbalimbali zinazofanywa na Serikali
 kupitia vyombo vyake vya ulinzi na usalama sambamba na kuwashirikisha 
wananchi kwa kuimarisha ulinzi na doria za mara kwa mara za 
kiitelijensia katika maeneo ya hifadhi.
Utalii
Katika
 kuongeza idadi ya watalii nchini, Wizara imeendelea kutekeleza shughuli
 mbali mbali ikiwa ni pamoja na kuimarisha ulinzi kwenye maeneo ya 
hifadhi, kuboresha miundo mbinu kwenye maeneo ya vivutio, kuanzisha 
huduma mpya za utalii pamoja na utangazaji.
Juhudi
 hizo zimewezesha ongezeko la watalii wa kimataifa kutoka 1,284,279 
mwaka 2016 hadi kufikia 1,327,143 mwaka 2017 sawa na ongezeko la 
asilimia 3.2.
Aidha,
 mapato yanayotokana na utalii yameongezeka kutoka Dola za Marekani 
bilioni 2.1 mwaka 2016 hadi Dola za Marekani bilioni 2.2 mwaka 2017.
Sekta
 hii ya utalii imetoa ajira takriban 500,000 za moja kwa moja na ajira 
nyingine milioni moja zisizo za moja kwa moja kwa mwaka.
Sekta hii pia inachangia takriban asilimia 17.5 ya Pato la Taifa na wastani wa asilimia 25 ya fedha zote za kigeni.
Aidha,
 Wizara imedhamiria kupanua wigo wa vivutio vya utalii nchini kwa 
kufungua utalii wa Kanda ya Kusini ili kuongeza idadi ya watalii na 
mapato ya Serikali. 
Kupitia
 dhamira hiyo Serikali imesaini mkopo wa masharti nafuu kutoka Benki ya 
Dunia wa Dola za Marekani milioni 150, sawa na takriban shilingi bilioni
 340 kwa ajili ya kutekeleza mradi wa Kusimamia Maliasili na Kuendeleza 
Utalii wa Ukanda wa Kusini –REGROW.
Mradi
 huu ambao maandalizi yake yalianza mwezi Novemba 2014 ulizinduliwa 
rasmi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia 
Suluhu Hassan tarehe 12 Februari, 2018 katika viwanja vya Kihesa Kilolo 
Mjini Iringa huku Kauli Mbiu yake ikiwa “Utalii kwa Maendeleo Endelevu- 
Karibu Kusini”.
Mama
 Samia alisema lengo la mradi huo ni kuongeza mchango wa sekta ya 
maliasili na utalii katika uchumi wa taifa kwa kuboresha vivutio vya 
utalii, miundombinu, usimamizi wa vivutio na kuongeza faida za kiuchumi 
kwa jamii zinazoishi jirani na maeneo ya hifadhi katika ukanda huo wa 
kusini.
Katika
 kuongeza jitihada za kutangaza utalii ndani na nje ya nchi, Wizara 
imeendelea kuongeza bajeti ya utangazaji ambapo Bodi ya Utalii Tanzania 
kwa mwaka wa fedha 2017/18 imeongezewa bajeti kufikia shilingi bilioni 
6.6 ikilinganishwa na shilingi bilioni 4.1 mwaka 2016/2017 na bilioni 
4.3 mwaka 2015/16.
Aidha,
 katika kufungua masoko mapya ya utalii nje ya nchi, Wizara inaangazia 
masoko mapya katika nchi za China, Israel, Urusi, Australia na nchi 
nyingine za Skandinavia.
Wananchi wanavyonufaika na uhifadhi 
Wizara
 ya Maliasili inaendelea na juhudi za kuhakikisha wananchi wanaoishi 
jirani na maeneo ya hifadhi wananufaika na rasilimali zilizopo. Kupitia 
Jumuiya za Hifadhi za Wanyamapori, jamii zinanufaika kwa kupata ajira, 
kitoweo, elimu, miradi ya kijamii na kuongeza kipato.
Hadi
 hivi sasa jumla ya Jumuiya za Hifadhi za Wanyamapori 38 zimeanzishwa. 
Aidha, wananchi wanaoishi jirani na misitu wananufaika kupitia miradi ya
 ufugaji nyuki ambapo kupitia uwezeshaji wa Mfuko wa Misitu Tanzania 
miradi 254 ya kuboresha kipato cha jamii zinazoishi pembezoni mwa misitu
 imetekelezwa.
Miradi
 hiyo ni ya ufugaji nyuki ambapo vikundi vya ufugaji nyuki 399 na watu 
binafsi 27 wamewezeshwa kupata mizinga ipatayo 11,730.
Udhibiti wa migogoro baina ya wananchi na hifadhi
Katika
 kudhibiti migogoro ya mipaka kati ya wananchi na maeneo jirani na 
hifadhi, Wizara kwa kushirikiana na Taasisi za Serikali na Wadau 
imeendelea kuhakiki mipaka yote ya maeneo ya hifadhi na kuweka alama za 
kudumu na mabango ya tahadhari.
Hadi
 kufikia mwezi Mei, 2017 vigingi 14,755 vimesimikwa sawa na asilimia 
62.4 ya vigingi 23,638 vinavyohitajika katika Hifadhi za Misitu, Mapori 
ya Akiba, Hifadhi za Taifa na Hifadhi ya Mamlaka ya Ngorongoro.
Aidha,
 kupitia program ya Panda Miti Kibiashara, Wizara imewezesha vijiji 48 
kuandaa Mipango ya Matumizi Bora ya Ardhi katika Wilaya za Ludewa, 
Madaba, Makete, Mufindi, Njombe Mjini, Njombe Vijijini, Kilolo na Nyasa.
Mikakati mipya chini ya Waziri wa Maliasili, Dk. Hamisi Kigwangalla
Aidha
 chini ya Uongozi Mpya wa Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi 
Kigwangalla ipo baadhi ya mikakati yake mipya inayolenga kutoa uelekeo 
mpya wa kuimarisha sekta Maliasili na Utalii nchini.
Dk.
 Kigwangalla anaeleza mikakati hiyo kuwa ni pamoja na kuanzisha kwa 
mwezi maalum wa Urithi wa Mtanzania (Tanzania Heritage Month) ambao 
utaadhimishwa mwezi Septemba kila mwaka, kuanzishwa kwa Makumbusho ya 
Marais Wastaafu waliotawala Tanzania mjini Dodoma na Kuboresha na 
kuendeleza utalii wa fukwe kwa kuanzisha Mamlaka ya Fukwe.
Mikakati mingine ni pamoja na kujenga makumbusho ya meno ya tembo katika miji ya Dar es Salaam, Dodoma, Arusha na Iringa pamoja na kutambua barabara iliyokuwa ikitumika katika biashara ya utumwa wakati wa ukoloni ili iweze kutumika kiutalii.
Akizungumzia
 migogoro ya mipaka iliyopo baina ya wananchi na maeneo ya hifadhi, Dk. 
Kigwangalla amesema Serikali itatatua migogoro hiyo kwa kushirikisha 
wananchi sambamba na kuwasaidia kutatua changamoto za msingi ambazo ni 
kuimarisha maeneo ya malisho ya mifugo, upatikanaji wa maji kwa ajili ya
 wananchi na mifugo, mpango bora wa matumizi ya ardhi na uendelezaji wa 
kilimo na ufugaji.
Kwa
 upande wa vitalu vya uwindaji wa kitalii, Dk. Kigwangalla amesema 
Serikali itafanya mabadiliko katika mfumo wa ugawaji vitalu vya uwindaji
 wa kitalii kutoka mfumo unaotumika hivi sasa wa Kamati “Administrative 
Allocation” na kutumia mfumo wa mnada “Auction”.
Lengo
 ikiwa ni kuongeza uwazi na kuruhusu nguvu ya soko kuamua bei ambapo 
mapato ya Serikali nayo yatatarajiwa kuongezeka maradufu. Ili kutekeleza
 hilo, sheria na kanuni zinafanyiwa marekebisho.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni