Waziri
 wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Seleman
 Jafo akiongea na wamachinga wakati  wa kufungua  Mkutano Mkuu wa 
Shirika la umoja wa wamachinga Tanzania- SHIUMA leo uliofanyika katika 
ukumbi wa shule ya Sekondari Dodoma, Jijini Dodoma.
 Waziri
 wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Seleman
 Jafo akiongea na wamachinga wakati  wa kufungua  Mkutano Mkuu wa 
Shirika la umoja wa wamachinga Tanzania- SHIUMA leo uliofanyika katika 
ukumbi wa shule ya Sekondari Dodoma, Jijini Dodoma.
Waziri
 wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Seleman
 Jafo  akiongea na baadhi ya viongozi wa shirika la umoja wa wamachinga 
Tanzania – SHIUMA leo alipokuwa akifungua Mkutano Mkuu uliofanyika 
katika ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Dodoma, Jijini Dodoma.
Na Mahmoud Ahmad,
Wakuu 
wa Wilaya wameagizwa kuzisimamia halmashauri nchini kuhakikisha kuwa 
zinatenga maeneo maalum ya kufanyia biashara ndogondogo (machinga) ili  
waweze kuendesha shughuli zao bila kuvunja sheria, kanuni na taratibu 
zilizowekwa na serikali. 
Agizo 
hilo limetolewa na Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na 
Serikali za Mitaa Mhe. Selemeni Jafo wakati akifungua Mkutano Mkuu wa 
Shirika la umoja wa wamachinga Tanzania – SHIUMA uliofanyika leo katika 
ukumbi wa shule ya Sekondari ya Dodoma, Jijini Dodoma.
Alisema
 Wakuu wa Wilaya wana wajibu wa kuratibu na kuhakikisha kuwa maeneo ya 
kufanyia bishara kwa wamachinga yanatengwa na Halmashauri ili 
kuwawezesha kufanya kazi zao kwa utaratibu bila kuvunja sheria za nchi. 
Aliongeza
 kuwa wamachinga ni watu muhimu katika kukuza uchumi wa Tanzania kwa 
kuwa wafanyabiashara wadogo ndio wanaoleta muunganiko wa watu katika 
kada mbalimbali wakiwemo wasomi wenye shahada, astashaada, kidato cha 
sita, kidato cha nne, darasa la saba na wasiosoma kabisa wote huunganika
 na kufanyabiashara kama wamachinga.
Alisema
 kati ya watanzania milioni 50, walioajiriwa serikalini na sekta ya umma
 ni 520,000, hivyo kundi kubwa ni la watu ambao ama wamejiajiri au 
wameajiriwa katika sekta binafsi. 
 
“Lakini
 kundi kubwa ni wale watu wanaojishughulisha kwa kutafuta riziki zao 
wenyewe ambao watu hao ndio unapata asilimia kubwa wako katika kundi la 
wamachinga,” alisema Mhe.Jafo na kuongeza:
“Utakuta
 mtu anafanyabishara katika mazingira magumu ambayo yanamfanya kila 
wakati kutokuwa na uhakika wa kupata kipato cha siku jambo ambalo 
linaathiri familia yake na kuongeza umaskini nchini, hivyo ifike mahali 
wakuu wa Wilaya waweke mikakati ya kuhakikisha wamachinga wote 
wanapatiwa maeneo bora ya kufanyia biashara ili wajikwamue kiuchumi,  
“alisisitiza Waziri 
Aliongeza
 kuwa Serikali imejiwekea mkakati wa kutengeneza masoko mazuri na ya 
kisasa kwa kuweza kuweka mazingira bora kwa wamachinga kufanya biashara 
zao katika maeneo stahiki.
Aidha 
Waziri Jafo alisema kuwa Viongozi wanatakiwa kutafakari na kutatua kero 
ya maeneo kwa ajili ya kufanyia biashara wamachinga, hivyo serikali 
imeanza mpango mkakati  wa ujenzi wa masoko mazuri ya kisasa ili 
wafanyabishara waweze kufanya kazi katika mazingira bora na tayari 
imetenga shilingi bilioni 149 kwa ajili ya ujenzi wa masoko, stendi za 
kisasa na viwanda vidogo.
“Nimetoa
 maagizo soko lolote litakalojengwa lazima mustakabali wa 
wafanyabiashara wadogo wadogo waliokuwepo awali umejulikana na kuwa 
kipaumbele kwa kupatiwa maeneo ya kufanyia biashara pindi majengo hayo 
yanapokamilika hivyo viongozi wa halmashauri wahakikishe wanatoa 
kipaumbele kwa wafanyabiashara waliokuwepo awali,” alisema Jafo.
 
Alisema
 kuwa Serikali imekuwa ikiwekeza katika miradi mikubwa ikidhani 
inawagusa maskini lakini kwa bahati mbaya masoko mengi yanayojengwa 
wanaonufaika ni watu wenye fedha na kuwaacha wafanyabiashara waliokuwepo
 awali kabla soko kujengwa. 
Hivyo 
nawaagiza Wakuu wa Wilaya kuhakikisha wananchi masikini wanapatiwa 
nafasi katika masoko hayo ili waweze kujiongezea kipato.Amewaagiza
 wakurugenzi wa Halmashauri wote nchini kuhakikisha kuwa kabla soko 
halijaanza kujengwa kufanyike tathmini ya wafanyabishara waliokuwepo 
awali ili wawe kipaumbele pale soko linapokamilika.
Wakati
 huohuo Mhe. Jafo amewataka wamachinga nchini kuhakikisha wanajiunga na 
bima iliyoboreshwa ili iwawezeshe kuwasaidia pale wanapokuwa wagonjwa 
wao na familia zao kwa kuwa afya ni uhai.



Hakuna maoni:
Chapisha Maoni