Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa 
akisalimiana na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla 
wakati alipowasili kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja kuzindua Maadhisho ya 
Wiki ya Mazingira, Mei 31, 2018. Wapili kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa 
Pwani, Mhandisi Evarest Ndikilo. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa 
akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Dar es salaam, Kate Kamba 
wakati alipowasili kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam 
kuzindua Wiki ya Mazingira, Mei 31, 2018. Wapili kushoto ni Waziri wa 
Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla na watatu kushoto ni Mkuu 
wa Mkoa wa Pwani , Mhandisi Evarest Ndikilo.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa 
akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Space 
Engineering Limited, Bw. Philip Mtui kuhusu mkaa uliotengenezwa kutokana
 na takataka na kufungashwa kwenye kiroba tayari kwa kuuzwa wakati 
alipotembelea banda la Kampuni hiyo kabla ya kuzindua Wiki ya Mazingira 
kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam, Mei 31, 2018. 
katikati ni Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi, Evarest Ndikilo.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa 
akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji  wa Kampuni ya  Space 
Engineering Limited, Bw. Philip Mtui kuhusu  mkaa uliotengenezwa kutoka 
na takataka na kufungashwa kwenye kiroba tayari kwa kuuzwa wakati 
alipotembelea banda la Kampuni hiyo kabla ya kuzindua Wiki ya Mazingira 
kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam, Mei 31, 2018. Kulia
 kwake ni Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi, Evarest Ndikilo na kushoto ni 
Meneja Mauzo wa kampuni hiyo, Neema Matemba.
Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa 
akipata Maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Edosama 
Hardware Limited, Edward Maduhu kuhusu bidhaa mbalimbali zinazotokana na
 miti ambazo zinatengenezwa na kampuni hiyo wakati alipotembelea mabada 
ya maonyesho  kabla ya kuzindua Wiki ya Mazingira kwenye Viwanja vya 
Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam Mei 31, 2018. Kulia ni Waziri wa Nchi, 
Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba na 
kushoto ni Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Dar es salaam, Kate Kamba.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa 
akipata Maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Edosama 
Hardware Limited, Edward Maduhu kuhusu bidhaa mbalimbali zinazotokana na
 miti ambazo zinatengenezwa na kampuni hiyo wakati alipotembelea mabada 
ya maonyesho kabla ya kuzindua Wiki ya Mazingira kwenye Viwanja vya 
Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam Mei 31, 2018. Kulia ni Waziri wa Nchi, 
Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa 
akimsikiliza Bibi Nimwagile Mwaijumba wakati alipotembelea banda la 
Kituo cha Utengenezaji magari cha Nyumbu  na kujionea mashine ya 
kutengeneza mkaa bora kwa kutumia takataka iliyobuniwa na kutengenezwa 
na kituo hicho. Waziri Mkuu alitembelea mabanda ya maonyesho  kabla ya 
kuzindua Wiki ya Mazingira kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es 
salaam, Mei 31, 2018. Watatu kulia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa
 Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba na wapili kulia ni Mkuu wa
 Mkoa wa Opwani Mhandisi, Evarest Ndikilo.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa 
akimsikiliza Mkurugenzi wa Kampuni ya JHS , David Mwendapole  wakati 
alipotoa maelezo kuhusu majiko makubwa yanayotumia  gesi kidogo  katika 
maonyesho ya Wiki ya Mazingira kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar
 es salaam, Mei 31, 2018. Wanne kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya 
Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa 
akizungumza wakati alipozindua Wiki ya Mazingira kwenye Viwanja vya 
Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam Mei 31, 2018.
Baadhi ya wananchi waliohudhuria 
katika maadhimisho ya wiki ya Mazingira wakimsikiliza Waziri Mkuu, 
Kassim Majaliwa wakati alipowahutubia kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja 
jijini Dar es salaam, Mei 31, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa 
akiagana na viongozi baada ya kuzindua Wiki ya Mazingira kwenye Viwanja 
vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam, Mei 30, 2018. Kutoka kushoto ni 
Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarest Ndikilo, Waziri wa Maliasili na 
Utalii, Dkt. Hamis Kigwangala, Mwenyekiti wa CC wa Mkoa wa Dar es alaam,
 Kate Kamba,Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Kisare Matiku Makori  na kulia ni 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January 
Makamba. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
………………
*Aagiza viongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam wabadilike
*Ataka wasimamie wananchi waachane na matumizi ya mkaa
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa 
ameziagiza Wizara, mashirika na taasisi zote za Serikali na binafsi 
zianze kutumia nishati mbadala ili kuondoa kabisa matumizi ya kuni na 
mkaa.
“Wizara, taasisi na mashirika yote
 ya Serikali na binafsi pamoja na vikundi vya uzalishaji wanaotumia 
nishati ya kuni na mkaa kwa ajili ya kupikia au shughuli za uzalishaji 
waanze kutumia nishati mbadala ili matumizi ya mkaa yaishe na 
ikiwezekana yatoweke kabisa,” amesema.
Ametoa agizo hilo leo 
(Alhamisi, Mei 31, 2018) wakati akizungumza na mamia ya wananchi na 
viongozi wa mkoa wa Dar es Salaam walioshiriki uzinduzi wa maadhimisho 
ya Siku ya Mazingira Duniani kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar 
es Salaam. Kaulimbiu ya mwaka huu ni: “Mkaa ni Gharama: Tumia Nishati 
Mbadala.”
Waziri Mkuu amesema teknolojia 
bora ya uzalishaji wa mkaa mbadala ambayo ameiona kwenye maonesho hayo, 
ikuzwe na kusambazwa kote nchini ili kuwawezesha wananchi walio wengi 
waachane na matumizi ya mkaa wa kawaida na badala yake watumie 
mkaa-mbadala kwa lengo la kuhifadhi misitu na kupunguza uharibifu wa 
mazingira.
Ili kufanikisha matumizi ya 
teknolojia hiyo, Waziri Mkuu amesema vibali vya ujenzi wa majengo 
makubwa na taasisi kama shule, vyuo, hospitali navyo pia vianze 
kuzingatia ufungaji wa mifumo ya nishati ya gesi kwa ajili ya matumizi 
ya kupikia ili kurahisisha upatikanaji na matumizi ya nishati mbadala 
katika taasisi na majengo makubwa.
“Wahandisi na wachoraji ramani za 
majengo waweke njia za kupitisha kwenye michoro yao ili ujenzi wa nyumba
 na majengo haya ukikamilika, watumiaji waweze kutumia teknolojia hiyo,”
 amesema.
Wakati huohuo, Waziri Mkuu amesema
 Mkoa wa Dar es Salaam ni lazima ubadilike na uachane na matumizi ya 
mkaa. Kwa mujibu wa takwimu zilizopo, mkoa huo unatumia tani 500,000 za 
mkaa kwa mwaka.
“Viongozi wa mkoa na wilaya 
ondokeni hapa na hili kama ajenda ya mkoa wa Dar es Salaam, mkaifanyie 
kazi na Wizara pia ifuatilie mmetekeleza kwa kiasi gani. Jitihada 
zilizofanywa na Jiji la Dar es Salaam kupitia kwa Mstahiki Meya, za 
kuanza kuwapa mtaji wajasiriamali hawa wanaotengeneza teknolojia mpya ni
 lazima ziigwe na nyie kwenye Manispaa zenu.”
“Meya ametoa fursa na 
amewaanzishia, na ninyi sasa endeleeni. Tengenezeni bajeti kupitia 
Mabaraza ya Madiwani na muwaunge mkono wajasiriamali wanaotengeneza haya
 majiko kwa kuwapa teknolojia hii kwenye maeneo yenu. Wanaotengeneza 
mashine za mkaa mbadala, wawezeshwe watengeneze mashine nyingi zaidi na 
zije kila Manispaa, ili kila Manispaa ianze kutumia teknonolojia hiyo 
kupikia,” alisisitiza.
Amewaagiza Wakuu wa Wilaya na 
Wakurugenzi wa Manispaa za Jiji la Dar es Salaam wafuatilie kwa karibu 
usambazaji wa teknolojia hiyo.
Kwa upande wake, Waziri wa Nchi 
Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), January Yusuf Makamba 
amesema hali ya mazingira hapa nchini ni mbaya licha ya kuwa haionekani 
kwa haraka na watu waishio mijini.
“Hali ya mazingira nchini mwetu ni
 mbaya sana na inawezekana watu wanaoishi Dar es Salaam hawaioni kwa 
haraka kwa sababu mahitaji yao yote wanayapata sokoni na madukani,” 
alisema.
“Wenzetu wa mikoani na vijijii 
wanaotegemea mvua na udongo wenye rutuba wanataabika kwa sababu kipato 
chao kinaathirika kutokana na uharibifu wa mazingira,” alisema.  
Alisema mazingira yanafungamana na
 utalii, kilimo, ufugaji, nishati, maji na kwamba maendeleo ya nchi pia 
yamefungamana moja kwa moja na mazingira. “Asilimia 90 ya Watanzania 
wanatumia kuni na mkaa kupikia lakini asilimia 70 ya mkaa wote 
unaozalishwa nchini Tanzania, unatumika jijini Dar es Salaam,” alisema.
Waziri Makamba alisema taasisi za 
Serikali kama vyuo, magereza, hospitali na shule zinaongoza kwa matumizi
 ya kuni na mkaa na hivyo kuchangia uharibifu mkubwa wa mazingira.
Akitoa mfano, alisema Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kina wanafunzi wapatao 30,000 na kinalazimika kuandaa milo mitatu kila siku.
“Chuo hiki kina migahawa tisa, 
kule nyuma kumejaa magogo ya kuni. Kuna mgahawa mmoja mdogo unatumia 
magunia 17 ya mkaa kwa siku, sasa huo mkubwa unatumia magunia mangapi?” 
alihoji.
Maadhimisho hayo yaliyozinduliwa 
leo, yataendelea hadi Juni 5, mwaka huu ambayo ni siku ya kilele. Pia 
wiki nzima kutakuwa na makongamano, midahalo na mjadala wa kitaifa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni