Arusha
Taasisi
 isiyokua ya kiserikali ya Wanaume inayojulikana kama Men At Work 
imeendesha zoezi la kuchangia damu kwa ajili ya kinamama wanaojifungua 
na majuruhi wanaonusurika na ajali na kufikishwa katika hospitali ya 
mkoa ya Mount Meru .
Mkurugenzi
 wa Taasisi hiyo Maxwell Stanslaus amesema kuwa wameamua kuwa wameamua 
kuchangia damu  kama mchango wanaume kujitoa kwa ajili ya jamii na 
kuisaidia jami kwasababu wanaume ni nguzo ya familia,jamii na taifa kwa 
ujumla.
Max aliwataka wanaume wote nchini kuwajibika na kuwa mstari wa mbele katika kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii .
“Kwa
 sasa  tumeamua kushirikiana na kitengo cha damu salama kuchangia damu 
ili kupunguza changamoto ya upungufu wa damu katika benki ya damu “ 
Alisema Max
Max
 alisema kuwa taasisi hiyo ina kazi kuwa ya kuwahasisha wanaume kuwa 
wawajibikaji na kushiriki katika nafasi za malezi  familia na jamii ili 
kujenga familia imara na hatimaye taifa imara.
Kwa
 upande wake Mwanachama wa Men At Work Rodgers Nelson alisema kuwa 
anajisikia faraja kuchangia damu  ili kusaidia kuokoa maisha ya kinamama
 wajawazito ambao hupoteza damu nyingi wakati wa kujifungua.
Naye
 Shemeji Melayeki  alieleza kuwa ni mara yake ya kwanza kutoa damu hivyo
 amewatoa hofu wananchi kutokua waoga wa kuchangia damu kwani zoezi hilo
 linafanyika kwa umakini na halina madhara yoyote.
Mkurugenzi 
wa Taasisi ya Wanaume ya Men at work Maxwell Stanslaus  akizungumza na 
Mkazi wa Arusha katika zoezi la uchangiaji wa damu lililoensheshwa ma 
taasisi yake.Picha na Ferdinand Shayo
Mwanachama wa Taasisi ya Wanaume ya Men at work akichangia damu
Mwanachama wa Taasisi ya Wanaume ya Men at work Rodgers  akichangia damu katika viwanja vya Sheikjh Amri Abeid
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni