MGUFULI ANAWATUMIKIA WANANCHI WOTE BILA KUJALI ITIKADI ZAO ZA VYAMA :MSIGWA


Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa amefagilia utendaji kazi wa Rais John Magufuli kwamba amekuwa akitekeleza majukumu yake bila kubagua vyama vya siasa, huku akitolea mfano jinsi fedha za miradi mbalimbali zinavyomiminika jimboni kwake

Mchungaji Msigwa ametoa kauli hiyo jana Mei 2, 2018 katika Ikulu ndogo ya Iringa kwenye hafla fupi ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na Rais Magufuli

Hata hivyo, Msigwa Alipoulizwa kuhusu video inayosambaa ikionyesha akimwagia sifa kiongozi mkuu huyo wa nchi, amesema ni kweli ila video hiyo imekatwa na kuna mambo aliyoyazungumza, ikiwamo wanachama mbalimbali wanaohamia CCM

Wakati akizungumza katika hafla hiyo Mchungaji Msigwa amesema, “Mheshimiwa Rais umekuwa ukisisitiza katika hotuba zako kuwa hujali vyama na hilo limekuwa likidhihirika hujali vyama. Umesaidia sana bahati mbaya hawakukupangia ratiba ya kufungua miradi, hela za kutoka kwako zimekuja nyingi.”

“Amezungumza Mahiga (Balozi Augustine-Waziri wa Mambo ya Nje) tuna barabara nzuri katika kipindi chako ambacho umekuwa rais. Tumejenga barabara ya lami mradi wa Benki ya Dunia kutoka Mlandege mpaka kwa mkuu wa wilaya karibu Sh3.5bilioni.”

Katika maelezo yake ya leo kuhusu kauli yake hiyo,  Mchungaji Msigwa amesema katika video hiyo, hakuna kipande ambacho aliwazungumzia watu wanaohama vyama, kubainisha kuwa wanaotoka upinzani kwenda CCM hawana sababu ya kufanya hivyo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni