wana kijiji wafikishwa mahakamani kwa kutokua na vyoo




 washtakiwa wa kosa la kutokua na vyoo wakiwa    katika mahakama ya wilaya ya Longido 
 
Wananchi 15 wakazi wa kijiji cha Gebailumbwa wilaya ya Longido,Mkoani Arusha wamepandishwa kizimbani katika mahakama ya wilaya hiyo wakikabiliwa na makosa matatu ya kutokuwa na vyoo na kusababisha mlipuko wa ugonjwa wa kipindu pindu.
Akisoma mashitaka hayo April 2 mwaka huu, mbele ya hakimu mfawizi wa mahakama hiyo,Aziza Temu,Mwendesha mashitaka wa jeshi la polisi wilayani hum
o,Anzulimu Mihella amesema kuwa,shtaka la kwanza na la pili linawakabili washtakiwa wote kwa pamoja.
 
Washtakiwa hao ni Oleulei Losinigi(50),Kirusu Taitai(48), Kelepu Kesonyi(35)Lazaro Parteye(38),Joshua Metui(20)Kamete Lemomo(25)Kimare Lamama(38)Lemomo Kokoyo(25)na Zacharia Kabamngasi(33).Wengine ni Paulo Lemomo(30),Kaika Ngatete(55)Thimotheo Kibangasi(37) na Moko Tataya(75)
 
Amesema mnamo mwaka 2016 na April 30 mwaka 2018 washtakiwa hao kwa pamoja walitenda kosa kwa kukaidi Amri halali ya kuchimba vyoo ,jambo ambalo ni kinyume na kifungu cha sheria namba 124 sura ya 16 ya mwaka 2009.
 
Washtakiwa hao waliokuwa wakiongozwa na mwanasheria wao,Nicholaus Senteu walikana mashtaka na hakimu Temu alidai dhamana ipo wazi kwa kila mshtakiwa kuwa na mdhamini mmoja ambaye ni mtumishi wa Umma mwenye kuweza kusaini bondi ya shilingi milioni 10 kila mmoja.

Hata hivyo washtakiwa hao walishindwa kutimiza masharti ya dhamana  na kurudishwa rumande katika gereza kuu la Kisongo jijini Arusha hadi kesi namba 38 ya mwaka 2018 itakapo kuja kwa ajili ya kutajwa tena Mei 16 mwaka huu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni