Muonekano wa ubavuni wa jengo la bweni la wanafunzi  
  moja ya chumba cha wanafunzi ndani ya bweni 
 korido la moja ya bweni litakalotumiwa na wanafunzi wa kidato cha tano 
 ujenzi wa jengo la utawala ukiendelea 
moja ya jengo la maabara ya kisayansi
 baadhi ya vifaa vya majaribio ka vitendo vilivyopo ndani  ya maabara ya sayansi
 baadhi ya vifaa kwaajili ya mafunzo kwa vitendo
Halmashauri
 ya Manispaa ya Kigamboni inatarajia kufungua kidato cha tano na sita 
Julai mwaka huu katika Shule ya Sekondari Nguva kwa kuwa na wanafunzi 
160 wa kiume pekee ikiwa na michepuo ya PCM,PCB,HGE na EGM. 
Mkurugenzi
 wa Manispaa ya Kigamboni Bw.Stephen Katemba amesema kuwa katika kutatua
 changamoto ya ukosefu wa Shule ya Sekondari yenye kidato cha tano na 
sita kwenye Halmashauri, na kutimiza maelekezo ya Serikali kwa kila 
Halmashauri kuwa na shule ya kidato cha tano na sita, Manispaa iliamua 
kuboresha miundombinu ya Shule ya Nguva ili iweze kukidhi mahitaji 
hayo. 
Aidha
 amesema kuwa mradi huu unatekelezwa kwa thamani ya shilingi 492,864,576
 kwa kushirikiana na Serikali kuu, ambapo Serikali kuu imeweza kuchangia
 kiasi cha shilingi 259,000,000 na vyanzo vya ndani vya Halmashauri ya 
Manispaa ya Kigamboni ilichangia shilingi 233,864.576. 
Mkurugenzi
 amesema kwamba ili kuhakikisha Shule ina hadhi ya kidato cha tano na 
sita kwa mujibu wa vigezo vya wizara, ujenzi wa mabweni mawili kwaajili 
ya wanafunzi, vyoo, ujenzi wa daharia ambao bado unaendelea, ujenzi wa 
madarasa manne na ununuzi wa madawati, ununuzi wa vitanda kwaajili ya 
mabweni ya wanafunzi, ukarabati wa maabara ya sayansi na ujenzi wa jengo
 la utawala linalojengwa kwa juhudi za Mkuu wa Mkoa Mh. Paul Makonda 
vimefanyika . 
Mkurugenzi
 amesema kuwa lengo kuu ni kuhakikisha masomo ya kidato cha tano na sita
 yanatolewa kwa watoto wanaomaliza kidato cha nne kwa shule za sekondari
 za Kigamboni. 
Kukamilika
 kwa mradi kutawezesha kuongeza idadi ya wanafunzi watakaojiunga na 
kidato cha tano na sita,kuchochea maendeleo ya elimu katika Halmashauri 
ya Manispaa ya Kigamboni kwa kutoa fursa pana kwa wanafunzi kujiunga na 
elimu ya juu. 
Ameongeza
 kuwa ujenzi wa bwalo la chakula litakalowawezesha wanafunzi kutumia 
kwaajili ya chakula linaendelea kujengwa kwa kushirikiana na wadau 
mbalimbali. 
Imeandaliwa na: 
Kitengo cha Teknolojia, Habari na Mawasiliano 
Halmshauri ya Manispaa ya Kigamboni 
13/04/2018 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni