NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.
WANAWAKE
 visiwani Zanzibar wameshauriwa kutumia vizuri fursa ya ujasiriamali kwa
 lengo la kujiongezea kipato na kujiajiri wenyewe.
Ushauri
 huo umetolewa na Mkurugenzi wa Taasisi ya New Vision Consortium (NVCT) 
Pily Khamis Lapda, amesema wanawake wengi hapa nchini wamekuwa wakifanya
 shughuli za ujasiriamali kwa mazoea jambo linalopelekea kushindwa 
kufikia malengo yao ya kumiliki mitaji mikubwa ya kibiashara.
Amesema
 zipo njia mbali mbali za kuwakomboa wanawake kiuchumi zikiwemo kupenda 
na kuamini shughuli za ujasiriamali kama nyenzo ya kujikomboa kiuchumi.Amewashauri
 wanawake nchini kujiamini pindi wanapoanzisha biashara zao sambamba na 
kujiwekea malengo ya kudumu ya kibiashara yatakayowasaidia kumiliki 
mitaji mikubwa ya kibiashara. 
Mkurugenzi
 huyo Pily, akizungumzia malengo ya taasisi yake inayoendesha na 
kusimamia mafunzo ya kuyajengea uwezo wa kitaaluma makundi mbali mbali 
ya kijamii ili kupata uwezo wa kutumia ipasavyo fursa za ujasiriamali 
wenye maendeleo.“Wanawake
 tuwe mstari wa mbele kujifunza mbinu mbali mbali za kujikwamua 
kiuchumi, pia tujitume na kuwa wabunifu katika biashara zetu ili nasi 
tuwe miongoni mwa wajasiriamali wa kimataifa.”, amesema Mkurugenzi huyo.
Akitoa
 mada ya Uvumbuzi binafsi, mtaalamu wa Saikolojia na maendeleo ya 
vijana, Joseph Mrindo amesema wanawake waliopo katika sekta ya 
ujasiriamali wanatakiwa kuondokana na dhana ya ujasiriamali mdogo mdogo 
kwani hali hiyo inasababisha kudumaa kiakili na kushindwa kufikia 
malengo yao ya kumiliki biashara kunwa na makapuni.
Ameeleza
 kuwa Zanzibar ni sehemu muhimu yenye fursa za kibiashara hivyo wanawake
 wanatakiwa kutumia nafasi hiyo kujiongeza kibiashara.Mtaalamu
 huyo, amewasihi wajasiriamali kufuata maelekezo na mbinu mbali mbali za
 maendeleo ya kibiashara ili wawe na mitaji mikubwa itakayowawezesha 
kupewa mikopo kwa wakati na benki mbali mbali nchini.
Naye 
mshiriki wa mafunzo hayo, Munawar Sleiman Mbarouk amesema miongoni mwa 
changamoto zinazowakabili wajasiria mali ni ukosefu wa mitaji na ujuzi 
wa kufanya biashara zenye tija kwa mjasiria mali mmoja mmoja na vikundi.Mafunzo
 hayo ya siku mbili yanatolewa na taasisi ya New vision consortium 
(NVCT)iliyopo Zanzibar na jumla ya washiriki 200 kutoka taasisi binafsi 
na za umma wanapewa ujuzi huo wa ujasiriamali.
Wadhamini wa mafunzo hayo ni pamoja na NMB, ZSSF, ZURA na IQUITY BANK
MKURUGENZI
 wa New vision consortium Pily Khamis Lapda(aliyekaa katikati) akifungua
 mafunzo ya siku mbili ya ujasiriamali kwa wanawake wa Zanzibar 
yaliyofanyika katika Skuli ya Haile-Sela-ssie.
BAADHI
 ya washiriki katika mafunzo hayo kutoka taasisi binafsi na za umma 
wakifuatilia kwa makini mada mbali mbali zilizowasilishwa katika mafunzo
 hayo, huko Skuli ya Haile-Sela-ssie.
MSHIRIKI
 wa mafunzo ambaye pia ni mjasiria mali kutoka U.WT. jimbo la Mwera 
Salama Mohamed Tahir akichangia mada ya uvumbuzi binafsi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni