Na Jumbe Ismailly, IKUNGI 
IDADI
 ya wakazi wa vijiji vya Kaugeri na Mduguyu,kata ya Mwaru,wilaya ya 
Ikungi waliokosa makazi kutokana na nyumba zao kuanguka kufuatia mvua 
kubwa zinazoendelea kunyesha Mkoani hapa zimeongezeka kutoka kaya 22 
zanye zaidi ya wakazi 154 hadi kufikia kaya 177 zenye zaidi ya wakazi 
700 baada ya nyumba189 kuanguka.
Ongezeko
 la idadi hiyo ya wakazi linatokana na mvua kubwa iliyonyesha apr,16 
hadi 18,mwaka huu na kusababisha mto kuacha njia yake na kulenga katika 
Kitongoji cha Mwasusu,na ndipo kaya 22 zenye zaidi ya wakazi 154 katika 
vijiji vya Kaugeri na Mduguyu,Kata ya Mwaru kukosa makazi baada ya 
nyumba 34 kuanguka.u
Ofisa
 Mtendaji wa Kata ya Mwaru,Hamisi Malongo alisema hayo alipokuwa akitoa 
taarifa za athari zilizotokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha hivi
 sasa Mkoani Singida na kuongeza kwamba pamoja na nyumba hizo vile vile 
makanisa matatu ya FPCT na AIC yalianguka kufuatia mvua hizo.
“Na
 tuliloligundua sisi kama viongozi kama serikali upande wa kata kwamba 
vijiji vya Kaugeri na Mduguyu ni vijiji vya mpakani na Mkoa wa Tabora 
ambavyo ndiyo bonde la Mto Wembere unapita kwa hiyo mvua inaponyesha 
pande zote za dunia kwa hiyo wao ni rahisi sana kuathirika na mvua 
hizo.”alisisitiza Malongo.
Naye
 Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Kaugeri,Laurence Bomba Torokoko 
akizungumzia hasara zilizotokana na mvua hizo alizitaja kuwa ni pamoja 
na nyumba 105 zenye wakazi 412 walikosa makazi kabisa ya kuishi na 
hekari 92 za mazao mbali mbali.
Madhara
 mengine kwa mujibu wa Torokoko magunia 334 ya mpunga na mtama,kuku 20 
na ng’ombe moja amba hatha hivyo alitumia fursa hiyo kuiomba serikali 
kuwasaidia familia zilizoathirika kutokana na mvua hizo ambazo bado 
zinaendelea kunyesha.
Kwa
 upande wao baadhi ya waathirika wa mvua hizo,Mchungaji,Hosea Eliudi 
licha ya kuishukuru serikali kwa msaada wa awali lakini hakusita kueleza
 changamoto zinazowakabili kwenye kambi hiyo kuwa ni hatari ya kuugua 
ugonjwa wa malaria kutokana na kuwepo kwa mbu wengi huku wakiwa hawana 
vyandarua baada ya walivyokuwa wakitumia kuangukiwa na nyumba zao.
Misaada
 pamoja na changamoto zingine kwa mujibu wa mchungaji huyo ni mahema 
makubwa yatakayoimarisha kambi hiyo kufanana na zile za wakimbizi na 
kuzitaja changamoto zingine kuwa ni kushindwa kuvuna kwa kuwa hawana 
sehemu ya kuhifadhi mazao yao.
Mashiri
 Masunga mkazi wa ni mmoja waathirika wa mafuriko ya mvua hizo kwa 
upande wake anaelekeza shutuma zake kwa Mbunge wa jimbo la Singida 
Magharibi,Elibariki Kingu kwamba licha ya kuwaahidi kuwapelekea kadi za 
CCM pamoja na maturubai tangu apr,23,mwaka huu lakini wamejikuta 
wakiende na matatizo ya kutokuwa na kifaa hicho muhimu kwa kujikinga na 
mvua.
Mmoja
 wa wananchi walioathirika kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha akiwa
 kwenye makazi yake mapya yaliyopo kitongoji cha Mwasusu,Kijiji cha 
Kaugeri akihofia wingu lililotanda kama alivyokutwa na kamera ya kituo 
hiki(Picha zote Na Jumbe Ismailly)
Baadhi
 ya wakazi wa vijiji vya Kaugeri na Mduguyu,kata ya Mwaru,wilayani 
Ikungi wakihamisha baadhdi ya vitu vilivyosalia kwenye makazi yao ya 
zamani na kuhamia kwenye eneo lililotengwa na serikali kwa ajili ya 
wahanga hao wa mafuriko yaliyotokana na mvua zilizonyesha kwa sisku tatu
 mfululizo na hivyo kusababisha zaidi ya wakazi 700 kukosa mahali pa 
kuishi
Ni
 Miundombinu ya barabara ya kutoka Mlandala kwenda kwenye Kitongoji cha 
Mwasusu,Kijiji cha Kaugeri sehemu iliyotengwa kwa ajili ya wahanga wa 
mafurriko ya mvua zilivyoharibika kutokana na mvua kubwa zinazoendelea 
kunyesha Mkoani Singida.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni