*Ahimiza vijana kusaka maarifa kwa nguvu zote ili wawe viongozi bora
*Ataka wazee kurithisha vijana yale yaliyofanywa na Mwalimu Nyerere
Na Said Mwishehe ,Globu ya jamii
WAZIRI
 wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano na Mazingira
 katika Serikali ya Awamu ya Tano Januari Makamba amesema vijana wengi 
nchini kwa sasa wamejaa taarifa badala ya 
maarifa.
Hivyo 
amesema ili vijana wawe viongozi bora na wanzuri kwa Taifa letu ni vema 
wakafanya juhudi na kuhakikisha wanapata maarifa ambayo yatakuwa dira na
 muelekeo kwa nchi yetu.January amesema hayo leo wakati wa Kongamabo la 
Kumbukizi ya Mwalimu Julius Nyerere ambayo imefanyika katika Chuo cha 
Kumbukumbu cha Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaa. 
Mada 
kuu kwenye kongamano inasema Kuelekea uchumi wa kati mchango wa Mwalimu 
Nyerere kuhusu amani,umoja wa kitaifa na uwajibikaji.Amesema yeye kama 
viongozi kijana ametumia kongamano hilo muhimu kuhusu mchango wa Mwalimu
 Nyerere katika ujenzi wa taifa hili na kwa sehemu kubwa aliongoza kwa 
maarifa makubwa na yenye tija kwa nchi yetu.
Hivyo 
amesema kwa vijana wote wa Tanzania hasa wanaotaka kuwa viongozi ni vema
 wakajikita kitafuta maarifa zaidi badala ya kujaza taarifa vichwani 
ambazo nyingine hazina tija.
"Taarifa
 inakuwezesha tu kuwa mzuri kwenye mazungunzo katika vijiwe vya kahawa 
na katika kupiga soga.Lakini ukiwa na maarifa yatakufanya kijana kuwa 
kiongozi bora kwa nchi yetu.Nimebahatika kwenda Butiama na nilipofika 
nilifanikiwa kuingia maktaba yake Mwalimu, utaona namna ambavyo 
amesoma vitabu vingi sana ili kuwa na maarifa mapana kwa ajili ya kuliongoza vema taifa letu,"amesema January.
Ametoa
 mwito kwa vijana nchini kuhakikisha wanatumia muda mwingi kusaka 
maarifa badala ya taarifa na kuongeza Mwalimu Nyerere alifika Dar es 
Salaam akiwa na umri wa miaka 32 lakini kutokana na maarifa yake wazee 
walimuamini na akawa Rais wa Tanu.
Amefafanua
 kwa bahati mbaya kwenye mitandao ya kijamii kwa sehemu kubwa vijana 
wanaangalia zaidi mambo ambayo hayana maana na kutoa mifano kwa kueleza 
wengi wanaangalia taarifa za wasanii."Nenda kwenye youtub kisha angalia 
hotuba za Mwalimu Nyerere ambayo zinazungumzia mambo mapana ya nchi 
yametazamwa na watu ngapi.
Kisha angalia mambo yanayohusu wasanii yametazamwa 
na 
watu wakangapi.Utaona taarifa za wasanii zinaangaliwa zaidi kuliko 
hotuba za Mwalimu ambazo ni muhimu kuangaliwa na kila kijana,"amesema.
Pia 
amesema vijana waliofanya kazi na Mwalimu Nyerere wametimiza wajibu wao 
kwa kuhakikisha wanajenga nchini na kuweka misingi imara ya umoja na 
mshikamano, hivyo swali ambalo vijana wa sasa wamepanga kufanya nini kwa
 ajili ya nchi yetu.Amefafanua Mwalimu Nyerere wakati wa uhai amewahi 
kutoa hutuba ambayo alizungumzia kuanza kuona nyufa,hivyo vijana waliopo
 leo lazima watafakari nyufa hizo bado zipo na nini wanafanya kiziziba.
Kuhusu
 umuhimu wa kukumbukizi ya Mwalimu ,January amesema ni muhimu kuwa na 
kongamano hilo kwani linatoa nafasi kwa vijana kufahamu Mwalimu Nyerere 
alifanya nini kwa ajili ya Taifa letu.
Baadhi
 ya wageni waalikwa na wanafunzi wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu 
kilichopo Kigamboni jijini Dar es Salaam wakifuatilia hotuba ya mgeni 
rasmi kwenye Kongamano la Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere January 
Makamba(hayupo pichani) leo.

Mgeni 
rasmi kwenye Kongamano la Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere January Makamba 
akiwa kwenye picha ya pamoja na wageni waalikwa na viongozi wa Chuo cha 
Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere baada ya kufungua rasmi kongamano hilo 
ambalo lilikuwa na mada mbalimbali. kongamano hilo limefanyika leo 
chuoni hapo


Hakuna maoni:
Chapisha Maoni