Baada ya miongo kadhaa ya minong´ono, uchunguzi na kesi
 kufuatiliwa kwa karibu, huenda msanii wa Kimarekani  Bill Cosby 
akaelekea gerezani akiwa na umri wa miaka 80 kwa makosa ya udhalilishaji
 wa kingono.
Msanii huyo wa vichekesho alipatikana na hatia  siku ya Alhamisi yya 
kumpa dawa za kulevya na kumdhalilisha kingono mfanyikazi wa Chuo Kikuu 
cha Temple Andrea Constand katika makazi yake yaliyoko Philadelphia 
mwezi Januari, 2004.
 Wanasheria wanawake  wameutaja uamuzi huo 
kuwa wa kihistoria. Vuguvugu kwenye mitandao lenye jina #MeToo, 
limethibitisha kuwa waliokuwa wakimtuhumu Cosby siku zote hawakuwa na 
makosa: Haiba yake ya uungwana sasa  imevurugwa .
 Lili Bernard, 
aliyesema kuwa Cosby alimdhalilisha kingono kabla ya kumpa nafasi katika
 kipindi chake maarufu cha "The Cosby Show" mwaka 1992, alijawa na jazba
 katika mahakama kiasi cha kugonga kichwa chake bila ya kukusudia kwenye
 meza iliyokuwa mbele yake.
 
"Nimezidiwa na furaha, alisema Bernard nje ya mahakama huku akidondokwa na machozi." Je, nimeamka? Huu ni muujiza."
 Zaidi ya wanawake 60 wamelalama kuhusu Cosby
 Uamuzi
 huo, wa kwanza unaomhusisha msanii anayetambulika katika kipindi cha  
#MeToo, inahujumu sifa za  msanii mkubwa aliyevuka mipaka ya rangi 
katika  jukwaa la kuigiza la  Hollywood na kubobea kwenye Televisheni .
 Ni
 moja ya kesi iliotokana na  visa vilivyowakumbuka zaidi ya wanawake 60 
waliodai kuwa Cosby aliwapa dawa za kuelevya na kisha kuwadhalilisha 
kingono kwa kipindi cha miongo mitano, lakini ambao kadhia zao 
hazikuaminika ama zilipuuzwa kabla ya kuanza kampeni kwenye mitandao ya 
kijamii yenye anwani #MeToo iliyoangazia dhulma za kingono 
zilizotekelezwa na wanaume wenye ushawishi mkubwa katika jamii.
 Cosby
 alitumbua macho maelezo ya jaji yakisomwa, lakini baadaye akapaza sauti
 akimpinga jaji Kevin Steele baada ya mwendesha mashtaka kutaka Cosby 
apelekwe gerezani mara moja.
 Mwendesha mashtaka aliambia mahakama
 kuwa Cosby ana ndege ya kibinafsi na huenda akiachiliwa akatoroka. 
Cosby alikanusha kwa hasira kuwa anamiliki ndege na kumtusi mwendesha 
mashtaka .
 Cosby alishtakiwa kwa makosa matatu ya udhalilishaji 
wa kingono, kila moja likiwa na kifungo cha kati ya miaka mitano hadi 10
 gerezani.
 Mashtaka hayo huenda yakajumlishwa ama kuunganishwa 
kwa ajili ya hukumu, lakini ikizingatiwa umri wa Cosby, kifungo chochote
 kinamaana kuwa huenda akafia gerezani.
 Cosby amesema kuwa atakata rufaa
 
Utekelezaji
 wa kifungo chake huenda ukafanyika katika kipindi cha miezi mitatu. 
Kabla ya hayo Cosby lazima afanyiwe uchunguzi kuthibitisha iwapo kuwa ni
 mtumiaji wa nguvu wa dhulma za kingono. Aidha atajiandikisha kuwa 
mkosaji wa kingono kwa kuzingatia sheria za Megan.
 Jopo la wanaume saba na wanawake watano lilishauriana kwa muda wa masaa 14 kabla ya kutoa uamuzi dhidi ya Cosby.
 Constand-
 45, mfanyikazi wa Chuo Kikuu cha Temple, alisema Cosby alimlemaza kwa 
kumpa tembe tatu kisha akakosa fahamu, kisha akamdhalilisha kingono kwa 
kutumia vidole vyake alipokuwa amelala hana nguvu za kukubali ama 
kukataa. Cosby anadai kuwa kitendo hicho kiliafikiwa na wote.
 Cosby
 aliupungia mkono umati ambao ulikuwa nje ya mahakama na kuingia kwenye 
gari lake na kuondoka bila ya kusema chochote. Wakili wake Tom Mesereau 
alitangaza, "vita havijakamilika" na kusema kuwa atakata rufaa.
 Mawakili
 wa upande Cosby wakiongozwa na Mesereau, aliyeshinda kesi dhidi ya 
Michael Jackson kuhusu kuwadhalilisha watoto kingono, walishambulia 
Constand wakati wa kesi hiyo huku wakimuita muongo ambaye alimsingizia 
Cosby kwa lengo la kutaka kuwa tajiri.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni