Na Munir Shemweta, Morogoro
Waziri
 wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi amesisitiza umuhimu wa 
kuwashirikisha watumishi katika mipango ya uendeshaji Taasisi kwa kuwa 
suala hilo lipo kisheria.
Aidha,
 alisema kwa miaka yote Serikali imekuwa ikisisitiza Taasisi kujenga na 
kutekeleza utaratibu wa kushirikisha watumishi na hali hiyo inatokana na
 ukweli kuwa palipo na watumishi wengi pana mawazo mengi.Profesa Kabudi 
alisema hayo mwishoni mwa wiki wakati akifungua mkutano wa kumi na tatu 
wa Baraza la Wafanyakazi wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania 
uliofanyika katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) 
mkoani Morogoro.
‘’Ushirikishwaji
 watumishi kwenye mipango ya uendeshaji ofisi unasaidia kupata mawazo 
mengi na mapya yanayoweza kurahisisha uendeshaji wa ofisi na kutoa fursa
 ya kusikiliza kero na changamoto kwenye uendeshaji wa Taasisi na 
kushirikiana katika kutafuta ufumbuzi’’ alisema profesa Kabudi.
Aliongeza
 kuwa, kwa kushirikiana na watumishi ni dhahiri wanapata morari wa 
kushiriki kikamilifu kwenye utekelezaji wa mipango ya taasisi ambayo wao
 wenyewe walishiriki kuiandaa.Waziri huyo wa Katiba na Sheria alisema, 
ushirikishwaji unafanywa kupitia baraza la wafanyakazi kwa kuwa baraza 
ni chombo kinachowashirikisha wafanyakazi katika kupanga , kusimamia na 
kutekeleza mipango mbalimbali inayohusu shughuli za kazi za Taasisi kama
 zilivyoainishwa katika sheria za nchi.
Kwa 
mujibu wa Profesa Kabudi, Mabaraza hutoa fursa kwa wafanyakazi kushiriki
 katika maamuzi mbalimbali na kuboresha uhusiano baina ya wafanyakazi na
 uongozi pamoja na mazingira ya utendaji hasa mahala pa kazi hivyo 
baraza ni chombo cha kuimarisha na kuboresha demokrasia mahala pa kazi.
Amewataka
 wajumbe wa baraza wa Tume ya Kurekebisha Sheria kuzingatia suala la 
nidhamu kazini, misingi ya kazi na kutekeleza majukumu kwa kuzingatia 
sheria, kanuni, taratibu. Aidha, alitaka uzembe kazini upigwe vita na 
suala la kufanya kazi kwa mazoea kukomeshwe na kubainisha 
kuwa,vipaumbele viwekwe katika kulinda rasilimali za Tume na kuwa na 
nidhamu katika matumizi ya fedha na mali zake.
Kwa 
upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi wa Tume ya Kurekebisha 
Sheria ambaye ni Katibu Mtendaji Tume Casmir Kyuki alisema katika 
kipindi cha Julai 2017 hadi Machi 2018 Tume yake imeweza kutekeleza 
majukumu yake kama yalivyoainishwa katika bajeti.
Ameyataja
 majukumu hayo kuwa ni kufanya mapitio ya Mfumo wa Sheria Unaosimamia 
Haki Jinai, Sheria ya Ushahidi, Uchambuzi wa Kesi za Mahakama ya Rufaa, 
Mfumo wa Sheria Unaosimamia Huduma ya Ustawi wa Jamii, Mfumo wa Sheria 
za Ufilisi pamoja na kutoa elimu ya sheria kwa umma.
Ameishukuru
 serikali kwa mabadiliko makubwa iliyoyafanya katika sekta ya sheria 
kupitia tangazo la serikali namba 48,49 na 50 ambapo yameleta muundo 
mpya kwa kuanzishwa Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka ya Jinai na ile ya 
Wakili Mkuu wa Serikali ili kuongeza tija na ufanisi katika utendaji 
kazi.
Waziri
 wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi akifungua mkutano wa 
Baraza la Wafanyakazi wa Tume ya Kurekebisha Sheria uliofanyika katika 
Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine, kushoto ni Katibu Mtendaji wa Tume Casmir
 Kyuki na kulia ni Katibu wa Baraza Ambokile Mwakasungula (Picha na 
Munir Shemweta-TUMESHERIA)
Katibu
 Mtendaji wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Casmir Kyuki (Kushoto) 
akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Waziri wa Katiba na Sheria
 Profesa Palamagamba Kabudi kufungua mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa
 Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania uliofanyika katika Chuo Kikuu cha 
Kilimo Sokoine mkoani Morogoro, kulia ni Katibu wa Baraza Ambokile 
Mwakasungula (Picha na Munir Shemweta-TUMESHERIA)
Waziri
 wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi akimsikiliza Katibu 
Msaidizi wa Tume ya Kurekebisha Sheria Khalist Luanda mara baada ya 
kufunguka mkutano wa Baraza la Wafanyakazi Tume ya Kurekebisha Sheria 
uliofanyika katika Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine mkoani Morogoro, 
katikati ni Katibu Msaidizi wa Tume (Idara ya Mapitio) Angelah Bahati 
(Picha na Munir Shemweta-TUMESHERIA)
Sehemu
 ya Wajumbe Baraza la Wafanyakazi la Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania
 wakimsikiliza Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi 
(hayupo pichani) wakati akifungua mkutano huo uliofanyika Chuo Kikuu cha
 Kilimo Sokoine mkoani Morogoro.
Waziri
 wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi akiwa katika picha ya 
pamoja na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi Tume ya Kurekebisha Sheria 
katika Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine mkoani Morogoro.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni