Mkurugenzi
 Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), Bw. Masha Mshomba 
(kulia), akipokea tunzo na cheti kutoka kwa Bw. Eric Shitindi katibu 
Mkuu Wizara ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu baada ya MFuko 
kushinda nafasi ya pili katika masuala ya Usalama na Afya Mahala pa Kazi
 katika maadhimisho ya Siku ya Usalama na Afya Mahala pa Kazi Duniani 
tarehe 28 Aprili katika Uwanja wa Kichangani Iringa.
MFUKO 
wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) umeibuka mshindi wa pili katika masuala 
ya usalama na afya mahala pa kazi katika maadhimisho ya siku ya usalama 
na afya mahala pa kazi nchini ambayo huadhimishwa duniani kote tarehe 28
 Aprili kila mwaka.
Maadhimisho
 haya huratibiwa na Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) 
nchini na kwa mwaka huu yamefanyika Mkoani Iringa yakitanguliwa na 
maonyesho kutoka kwa wadau kuanzia tarehe 26 Aprili na kufikia kileleni 
leo tarehe 29.
Mgeni 
Rasmi katika kilele cha Siku ya Usalama na Afya Mahala pa Kazi Duniani 
Mhe. Jenista Mhagama (Mb) Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, 
Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu ameipongeza WCF kwa 
ushindi walioupata na kuwasihi kuendelea kutoa elimu kwa wadau wake. 
Kwa 
upande wake Mkurugenzi Mkuu wa WCF Masha Mshomba, amefafanua kuwa moja 
ya malengo ya uanzishwaji wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi ni kukuza na
 kuendeleza mbinu za kuzuia ajali, magonjwa ama vifo mahala pa kazi. 
Mshomba ametoa ufafanuzi huo leo katika viwanja vya Kichangani mkoani 
Iringa baada ya kupokea tuzo na cheti cha Mshindi wa pili katika masuala
 ya afya ya usalama mahala pa kazi. 
Aidha,
 akikabidhi tunzo hiyo kwa niaba ya Mgeni Rasmi, Katibu Mkuu Wizara ya 
Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu Bw. Eric Shitindi ameupongeza Mfuko
 kwa kuendelea kufanya kazi vizuri katika nyanja tofauti tofauti pamoja 
na kwamba hauna miaka mingi sana toka uanzishwe. “Tunajivunia sana kuona
 ya kwamba Mfuko umeweza kulipa fidia stahiki kwa wakati, kitu ambacho 
kilikuwa changamoto hapo awali” Aidha, pongezi zangu ziwafikie kwa 
kuanzisha mifumo inayoboresha huduma kwa waajili na waajiliwa wote 
ikiwemo mifumo ya ki- electroniki inayowazezesha waajili kujisajili, 
kulipia michango na kufuatilia michango yao. 
Mfuko 
umehitimisha maadhimisho ya siku ya usalama na afya mahala pa kazi 
katika Mkoa wa Iringa na unajiandaaa na semina ya wadau itakayofanyika 
tarehe 30 Aprili na hatimaye kushiriki katika maadhimisho ya Siku ya 
Wafanyakazi Duniani Tarehe 01 May 2018. 
Katikati
 Bw. Eric Shitindi Katibu Mkuu Wizara ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye 
Ulemavu akiwa kwenye picha ya pamoja na wafanyakazi wa Mfuko baada ya 
kupokea tunzo na cheti katika maadhimisho ya Siku ya Usalama na Afya 
Mahala pa Kazi katika Uwanja wa Kichangani Iringa. (Akishikilia kombe 
pamoja na Bw. Shitindi ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa 
Wafanyakazi Bw. Masha Mshomba
Bw. 
Ibrahim Mussa Afisa Madai Mwandamizi – WCF akimhudumia mteja 
aliyetembelea banda ya WCF katika maonyesho yaliyofanyika katika viwanja
 vya Kichangani Iringa.
Bw. Masha Mshomba akionyesha tuzo na cheti ambavyo Mfuko umetunukiwa.
Mkurugenzi
 wa Tiba na Tathmini wa WCF, Dkt. Abdulsalaam Omar (wapili kushoto), 
Mkurugenzi wa Uendeshaji Bw. Anselim Peter wakiwa ameshika tuzo hiyo 
huku, Meneja Tathmini ya Usalama na Afya mahala pa Kazi wa Mfuko huo, 
Bi. Naanjela Msangi, (kulia) na Afisa Mkuu wa Matekelezo, Bi. Amina 
Likungwala, wakionyesha vyeti vya ushindi wa pili na cha ushiriki.
Mkurugenzi
 wa Tiba na Tathmini wa WCF, Dkt. Abdulsalaam Omar (katikati), akiwa 
ameshika tuzo hiyo huku, Meneja Tathmini ya Usalama na Afya mahala pa 
Kazi wa Mfuko huo, Bi. Naanjela Msangi, (kulia) na Afisa Mkuu wa 
Matekelezo, Bi. Amina Likungwala, wakionyesha vyeti vya ushindi wa pili 
na cha ushiriki.
Afisa Uhusiano Mwandamizi wa WCF, Bw. Fulgence Sebera, akizungumza 





Hakuna maoni:
Chapisha Maoni