Makamu
 wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan 
ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM akizindua Siku ya Wanawake wa 
Mfano Tanzania iliyoandaliwa na Umoja wa wanawake wa Tanzania (UWT) 
katika ukumbi wa PTA, jijini Dar es Salaam 
Mama
 Fatma Karume akionyesha juu tuzo ya Mwanamke wa Mfano Tanzania ikiwa 
sehemu ya kutambua mchango wake katika harakati za Mapinduzi ambapo yeye
 alikuwa mke wa Rais wa kwanza wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe.
 Abeid Aman Karume 
Makamu
 wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan 
akimkabidhi tuzo ya Mwanamke wa Mfano mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya 
Nne Mama Salma Kikwete. 
Spika
 Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Mhe. Anna Makinda akionyesha 
juu Tuzo yake ya Mwanamke wa Mfano mara baada ya kukabidhiwa na Makamu 
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan. 
Mama
 Fatma Karume mke wa Rais wa kwanza wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
 akitoa nasaha zake mara baada ya kupokea tuzo ya Mwanamke wa Mfano 
iliyoandaliwa na Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT). 
Picha na Ofisi ya Makamu 
……………….. 
Makamu
 wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan 
amesema Wanawake walikuwa na mchango mkubwa katika harakati za Uhuru wan
 chi hii. 
Makamu
 wa Rais ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa Siku ya Mwanamke wa Mfano 
Tanzania iliyoandaliwa na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) 
Makamu
 wa Rais alisema Ni dhahiri kuwa wanawake walikuwa na mchango mkubwa 
sana. Walifanya kazi kubwa katika uhamasishaji, malezi ya watoto na 
vijana na kusimama bega kwa bega na kuunga mkono wanaume waliokuwa 
mstari wa mbele katika mapambano. Walifanya mengi nyuma ya pazia ambayo 
yalikuwa na mchango mkubwa katika Taifa letu. Mapenzi yao, subira yao na
 mchango wao wa hali na mali ndio uliowapa nafasi wanaume kufanikisha 
harakati za uhuru kwa kuwa wanawake waliwapa wepesi kwa kuwapunguzia 
mzigo mzito uliokuwa mabegani mwao. Haiyumkini, katika ngao yetu ya 
Taifa, ikatambua nafasi ya mwanamke kwa kuwekwa sambamba na mwanaume. 
Makamu
 wa Rais aliendelea kusema kutokana na kazi kubwa ya wanawake jasiri na 
mashujaa waliotutangulia, wanawake wa nchi yetu wameendelea kutoa 
mchango mkubwa katika Uongozi katika nchi yetu na nje ya mipaka yake. 
Makamu
 wa Rais alitoa wito kwa Wanawake na kusema Tuzo za “Mwanamke wa Mfano 
Tanzania” ziwe chachu yetu Wanawake katika kuchapa kazi, kuungana, 
kushikamana katika kuleta maendeleo miongoni mwetu na jamii nzima ya 
Watanzania. Sisi wanawake ni nusu ya watu wote nchini. Sisi tukijiongeza
 tukaendelea, kaya zetu zinaendelea na hatimaye nchi inaendelea. 
Makamu
 wa Rais aliwataka Umoja wa wanawake Tanzania (UWT) kuchukua jukumu lenu
 la kuwasemea, kuwatetea na kuwaunganisha wanawake wote wa Tanzania wana
 CCM, wasio wana CCM na wasio na vyama. Ndio wajibu wa UWT mliopewa na 
Katiba ya CCM. Katika nchi yetu, hamna chombo chochote kikubwa cha 
kuwaunganisha wanawake isipokuwa ninyi. Nawakumbusha kuwa nanyi 
mnatazamwa na wanawake wa nchi yetu. 
Jumla ya Tuzo 26 za Mwanamke wa Mfano zilitolewa .

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni