RC Gambo afiwa na Mama yake


Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amefiwa na mama yake mzazi usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya The Madras Medical Mission – Chennai nchini India alipokuwa akipatiwa matibabu.

RC Gambo kupitia mtao wake wa Instagram amethibitisha kifo hicho huku akieleza kuwa anahiaji maombi kwasababu huo ni mtihani mzito sana kwake.

"Kwa masikitiko na uchungu mkubwa napenda kutangaza kifo Cha Mama yangu Mzazi ( Mama aliyenilea kwa kuuza uji) kilichotokea usiku wa leo kwenye hospitali ya The Madras Medical Mission – Chennai nchini India! 

"Kama mtoto nilijitahidi kufanya kila lililowezekana ikiwa ni pamoja na kumpeleka Afrika Kusini kwa matibabu kabla ya India. Ni Imani yangu kuwa hata Mungu atakubali kuwa kama binadamu nilifanya kila lililowezekana Ila yeye kampenda zaidi! Niombeeni sana maana mtihani huu ni mzito sana kwangu sidhani kama nita uhimili!"

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni