Watafiti
 wa Kodi Barani Afrika wameshauriwa kuimarisha mtandao wao ili kuweza 
kusaidiana kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili katika jitihada 
zao za kufanya utafiti.
Ushauri
 huo umetolewa na Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa Mamlaka ya
 Mapato Tanzania (TRA) Bw. Michael John wakati akifunga warsha ya 
mafunzo ya kuwajengea uwezo wajumbe wa Mtandao wa Watafiti wa Kodi 
Afrika (ATRN) ambayo imeandaliwa na Taasisi ya Usimamizi wa Kodi Barani 
Afrika (ATAF) kwa kushirikiana na Chuo cha Kodi (ITA).
Bw.
 Michael amesema kwamba watafiti hao wanategemewa sana na mamlaka za 
mapato wanazoziwakilisha hivyo kuwataka kutumia ujuzi wa utafiti 
walioupata wakati wa mafunzo hayo ya siku nne kutatua changamoto 
mbalimbali na kuziongezea uwezo mamlaka za mapato barani Afrika hivyo 
kupelekea kuongeza makusanyo.
“Nina
 imani kwamba baada ya mafunzo haya mtaendelea kushirikiana kupitia 
mtandao wenu ili kwa pamoja mtimize lengo lenu la kutatua changamoto 
katika utekelezaji wa taratibu, sheria na sera za kodi barani Afrika 
kupitia utafiti mtakaoufanya”.Aidha
 amewataka watafiti hao kuzitumia vyema nyenzo za ukusanyaji na 
uchambuzi wa taarifa ambazo wamepatiwa wakati wa mafunzo hayo ambayo 
yamefanyika Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
 huyo wa Rasilimali Watu na Utawala ameipongeza Taasisi ya Kodi Barani 
Afrika pamoja na Chuo cha Kodi kwa kuandaa na kufanikisha mafunzo hayo 
ambayo ni muhimu katika utendaji wa usimamizi wa Kodi barani Afrika.
Naye
 Mkuu wa Chuo cha Kodi Pro. Isaya Jairo ameishukuru ATAF na TRA kwa 
kukiamini Chuo cha Kodi kuendesha mafunzo kwa watafiti ambao wametoka 
nchi mbalimbali za Afrika. Ambapo pia amewapongeza washiriki hao kwa 
kupatiwa nafasi kushiriki mafunzo hayo akisema kwamba ushiriki wao 
unadhihirisha utayari wa mamlaka za mapato barani Afrika kutatua 
changamoto zilizopo kwa kuwa na watafiti wenye weledi na ujuzi.
Awali
 akifungua mafunzo hayo, kwa niaba ya Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato
 Tanzania, Kaimu Kamishna wa Walipakodi Wakubwa Bw. Alfred Mregi alisema
 kwamba Usimamizi wa Kodi katika Afrika unakabiliwa na changamoto 
mbalimbali ambazo watafiti wanategemewa kuzitatua ili taasisi 
zinazosimamia mapato Afrika ziwe rafiki kwa walipakodi na hatimaye 
kuongeza makusanyo ya mapato ya ndani.
“Tunawategemea
 nyinyi kufanya utafiti wa mifumo ya kodi na kutoa suluhisho na 
mapendekezo kwa watunga sera na wasimamizi wa kodi”, alisema Bw. Mregi.
Warsha
 ya mafunzo kwa Mtandao wa Watafiti Afrika iliwashirikisha watafiti 
kutoka baadhi ya nchi za Afrika ambao mapendekezo yao ya utafiti 
yamekidhi vigezo kwa mujibu wa Taasisi ya Usimamizi wa Kodi Barani 
Afrika ambayo inaratibu Mtandao wa Wasimamizi wa Kodi Afrika kwa lengo 
la kuwajengea uwezo waafrika kufanya utafiti katika usimamizi, sheria na
 sera za kodi na kuwaunganisha watafiti hao na wanataaluma.
Washiriki
 wa warsha hii ambayo ni ya Tatu kufanyika, wameishukuru ATAF na Chuo 
cha Kodi kwa kuendesha mafunzo hayo wakisema kwamba imewapa uelewa zaidi
 wa kuendelea na utafiti wao.
Mafunzo
 hayo ambayo yaliendeshwa kwa lugha tatu: Kireno, Kifaransa na 
Kiingereza yaliwashirikisha washiriki 24 kutoka, Jamhuri ya Kidemokrasi 
ya Kongo, Niger, Msumbiji, Zambia, Zimbabwe, Togo, Benin, Cape Verde, 
Tunisia, Ivory Coast, Kenya na Tanzania.
Mkurugenzi
 wa Rasilimali Watu na Utawala wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. 
Michael John akimkabidhi mshiriki kutoka Tunisia Bw. Jabali Belhanssen 
cheti cha ushiriki wa mafunzo ya utafiti ambayo yafanyika jijini Dar es 
Salaam kwa ushirikiano wa Taasisi ya Usimamizi wa Kodi Afrika (ATAF) na 
Chuo cha Kodi (IAT). Wengine kutoka kushoto ni Mkuu wa Chuo cha Kodi 
(ITA) Prof. Isaya Jairo, Naibu Mkuu wa Chuo Taaluma na Utafiti Dr. Lewis
 Ishemoi na Mwakilishi ATAF Bw. Eugenio Bras.
Mkurugenzi
 wa Rasilimali Watu na Utawala wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. 
Michael John (katikati) akifuatilia matukio wakati wa kufunga na 
kukabidhi vyeti kwa washiriki wa warsha ya mafunzo kwa Mtandao wa 
Watafiti wa Kodi Afrika (ATRN) ambayo imefanyika jijini Dar es salaam. 
Wengina kutoka kushoto ni; Mkufunzi wa mafunzo hayo Prof. Nicaise Mede 
kutoka Benin, Mkuu wa Chuo cha Kodi (ITA) Prof. Isaya Jairo, Naibu Mkuu 
wa Chuo cha Kodi Taaluma na Utafiti Dr. Lewis Ishemoi na Mwakilishi wa 
Taasisi ya Utafiti Barani Afrika (ATAF) Bw. Eugenio Bras.
Baadhi
 ya washiriki wa Warsha ya Mafunzo kwa Mtandao wa Watafiti wa Kodi 
Afrika (ATRN) waliosimama wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa
 Rasilimali Watu na Utawala wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. 
Michael John (aliyekaa katikati) baada ya kufunga mafunzo hayo. Wengine 
kutoka kulia ni, Mwakilishi wa Taasisi ya Utafiti Barani Afrika (ATAF) 
Bw. Eugenio Bras, Naibu Mkuu wa Chuo cha Kodi Taaluma na Utafiti Dr. 
Lewis Ishemoi, Mkuu wa Chuo cha Kodi (ITA) Prof. Isaya Jairo na Mkufunzi
 wa mafunzo hayo Prof. Nicaise Mede kutoka Benin

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni