Waziri
 wa Nchi Ofisi (Sera, Bunge, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. 
Jenista Mhagama akizungumza na baadhi ya washiriki wa maonesho wakati wa
 maadhimisho ya Siku ya Afya na Usalama Mahali Pa Kazi Duniani Aprili 
28, 2018 iliyoadhimishwa Kitaifa Mkoani Iringa.
Waziri
 wa Nchi Ofisi (Sera, Bunge, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. 
Jenista Mhagama akiwasili katika Viwanja vya Kichangani Mkoani Iringa 
wakati wa maadhimisho ya Siku ya Afya na Usalama Mahali Pa Kazi Duniani 
Aprili 28, 2018. 
Waziri
 wa Nchi Ofisi (Sera, Bunge, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. 
Jenista Mhagama akitia saini katika kitabu cha wageni alipotembelea 
banda la maonesho la OSHA wakati wa maadhimisho ya Siku ya Afya na 
Usalama Mahali Pa Kazi Duniani Aprili 28, 2018 Iringa. 
Waziri
 wa Nchi Ofisi (Sera, Bunge, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. 
Jenista Mhagama akiangalia mfano wa namna bora ya kumuokoa mfanyakazi 
pindi apatapo ajari sehemu ya kazi wakati wa maadhimisho ya Siku ya Afya
 na Usalama Mahali Pa Kazi Duniani Aprili 28, 2018 Iringa. 
Waziri
 wa Nchi Ofisi (Sera, Bunge, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. 
Jenista Mhagama akizungumza na Mzee Juma Nyinge aliyetembelea katika 
mabanda ya maonesho wakati wa Siku ya Afya na Usalama Mahali Pa Kazi 
Duniani Aprili 28, 2018. 
Afisa
 Mahusiano na jamii kutoka Kampuni ya Acacia Bi. Agripina Joseph akitoa 
maelezo kwa Waziri wa Nchi Ofisi (Sera, Bunge, Vijana, Ajira na Watu 
wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama alipotembelea banda lao wakati wa 
maadhimisho ya Siku ya Afya na Usalama Mahali Pa Kazi Duniani. 
Waziri
 wa Nchi Ofisi (Sera, Bunge, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. 
Jenista Mhagama akiuliza swali kwa Afisa Usalama kazini Bw. Mlewa 
Mustapha kutoka Mgodi wa Buzwagi wakati wa maadhimisho ya Siku ya Afya 
na Usalama Mahali Pa Kazi Duniani. 
Waziri
 wa Nchi Ofisi (Sera, Bunge, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. 
Jenista Mhagama akipokea zawadi kutoka kwa Kampuni ya Acacia 
waliposhiriki katika maonesho ya kuadhimisha Siku ya Afya na Usalama 
Mahali Pa Kazi Duniani mkoani Iringa. 
Mwalimu
 wa wasioona Steven Changalo akiandika jina la mhe.Waziri Mhagama kwa 
kutumia vifaa wezeshi alipotembelea banda la Chama cha Walimu Tanzania 
(CWT) katika maadhimisho ya Siku ya Afya na Usalama Mahali Pa Kazi 
Duniani mkoani Iringa. 
Waziri
 wa Nchi Ofisi (Sera, Bunge, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. 
Jenista Mhagama akiteta jambo na Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw.Erick 
Shitindi anayeshungulikia Kazi,Ajira, Vijana na wenye ulemavu. 
Kaimu
 Mtendaji Mkuu OSHA Bi.Khadija Mwenda akizungumza jambo wakati wa Kilele
 cha Siku ya Afya na Usalama Mahali Pa Kazi Duniani yaliyoadhimishwa 
mkoani Iringa. 
Katibu
 Mkuu wa Ofisi hiyo Bw.Erick Shitindi anayeshungulikia Kazi,Ajira, 
Vijana na wenye ulemavu akitoa salamu kwa washiriki wa Maadhimisho ya 
Siku ya Afya na Usalama Mahali Pa Kazi Duniani yaliyofanyika mkoani 
Iringa. 
Waziri
 wa Nchi Ofisi (Sera, Bunge, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. 
Jenista Mhagama akitoa vyeti kwa washindi wa maonesho ya Siku ya Afya na
 Usalama Mahali Pa Kazi Duniani yaliyofanyika mkoani Iringa. 
Waziri
 wa Nchi Ofisi (Sera, Bunge, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. 
Jenista Mhagama akihutubia wananchi na washiriki waliohudhuria wakati 
Maadhimisho ya Siku ya Afya na Usalama Mahali Pa Kazi Duniani 
yaliyofanyika mkoani Iringa. 
Waziri
 wa Nchi Ofisi (Sera, Bunge, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. 
Jenista Mhagama (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na 
wafanyakazi wa OSHA pamoja na watendaji wa Idara ya Kazi, Ajira, Vijana 
na Wenye Ulemavu wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Afya na Usalama Mahali
 Pa Kazi Duniani yaliyofanyika mkoani Iringa. (PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU 
Serikali
 imedhamiria kuendelea kukomesha ajira hatarishi za watoto ili 
kuhakikisha kuwa watoto wanalindwa na kuwapa nafasi stahiki kulingana na
 sheria na kanuni zilizopo nchini. 
Hayo 
yameelezwa na Waziri wa Nchi Ofisi (Sera, Bunge, Vijana, Ajira na Watu 
wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama alipohudhuria katika kilele cha Siku
 ya Afya na Usalama Mahali Pa Kazi Duniani inayoadhimishwa kila mwaka 
tarehe 28 Aprili ambapo Kitaifa ilifanyika Mkoani Iringa. 
Waziri
 alieleza kuwa, katika mapambano haya ya ajira hatarishi kwa watoto ni 
moja ya utekelezaji wa kampeni zinazolenga kuharakisha utekeleezaji wa 
vipaumbele vilivyomo kwenye lengo namba (8) la Maendeleo Endelevu ya 
Umoja wa Mataifa ambalo ni kuboresha mazingira ya wafanyakazi na 
kukomesha ajira mbaya kwa watoto. 
“Tuendelee
 kupiga vita ajira mbaya kwa watoto kwa kuzingatia kampeni zilizopo hasa
 ile ya kuboresha mazingira ya wafanyakazi ifikapo mwaka 2030 pamoja na 
kukomesha ajira mbaya za watoto ifikapo mwaka 2025,” alisema Waziri 
Waziri
 aliongezea kuwa katika kuhakikisha watoto wanakuwa na mazingira salama ,
 Lazima kuwe na mikakati ya pamoja baina ya utatu katika masuala ya kazi
 na ajira ikiwemo na kujenga utamaduni wa kujikinga na vihatarishi 
sehemu za kazi vinavyoweza kusababisha kuhatarisha afya na usalama wa 
wafanyakazi. 
Aidha 
kama Taifa lazima tuoneshe umuhimu wa kuhakikisha kampeni hii inakuwa na
 matokeo chanya na kuendelea kuwa na Taifa lenye maendeleo. 
Waziri
 aliongezea kuwa kulingana na Matokeo ya Utafiti wa Mtakwimu Mkuu wa 
Serikali uliofanyika mwaka 2014 na matokeo yake kuchapishwa mwaka 2016 
ulibainisha kuwa, hali ya ajira hatarishi za watoto kuzidi kuwa mbaya 
zaidi katika sehemu za mashambani, sekta ya madini, misitu na uvuvi. 
“Kwa 
mujibu wa taarifa za Mtakwimu Mkuu wa Serikali za mwaka 2014 zilibaini 
kuwa watoto wenye umri kati ya miaka 5-17 walioko kwenye ajira ni 
takribani milioni 4.2 ambayo ni asilimia 28.8 ya wafanyakazi wote na 
kati ya hao asilimia 21.5 wako kwenye ajira hatarishi hususan sehemu za 
mashambani ambako asilimia 35.6 ya wafanyakazi wote ni 
watoto”,alisisitiza Mhe.Waziri 
Kwa 
upande wake Kaimu Mtendaji Mkuu wa OSHA, Khadija Mwenda alieleza kuwa 
wataendelea kutekeleza majukumu yao kwa kuhakikisha sheria zilizopo 
zinafuatwa bila kukiukwa hususan kwa makundi maalum iliwemo yale ya 
vijana na makundi ya watu wenye ulemavu. 
“kwa 
kuwa Vijana wadogo ndiyo nguvu kazi ya taifa hivyo wanastahiri kulindwa 
na kuangaliwa kwa jicho la pekee ili kuwa na kizazi endelevu,”alisema 
Mwenda 
AWALI 
Aprili
 28 ya kila mwaka ni siku ya Kimataifa ya kuadhimisha masuala ya Afya na
 Usalama Mahali Pa Kazi, ambapo huwa na Kauli Mbiu inayotumika duniani 
kote ambayo inatolewa na Shirika la Kazi la Duniani.Kauli mbiu ya mwaka 
huu ni “Kizazi Salama chenye Afya – Generation Safe and 
Health”.Kaulimbiu hiyo ili kuendana na mazingira ya nchi yetu 
iliboreshwa na kuwa “Kizazi Salama Chenye Afya kwa Uchumi wa Viwanda 
–Generation Safe and Health for Industrial Economy”.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni