MAHAKAMA YA TANZANIA KUANZISHA KITUO MAALUM CHA MIRATHI

NA MAGRETH   KINABO – MAELEZO

MAHAKAMA ya Tanzania, ina mpango wa kuanzisha  Kituo  maalum   kitakachoshughulikia  masuala ya mirathi ili kuweza kusogeza   huduma za masuala ya mirathi  kwa wananchi, ikiwa ni hatua ya kuwapunguzia gharama za fedha  wanazozitumia na muda wanaoutumia.
 Kutokana  na  eneo la mirathi limeonekana  kuwa na changamoto nyingi na hivyo kuhitaji mtazamo wa pekee Mahakama  inaanzisha,  Mpango huo ili kuongeza  ufanisi na  katika kushughulikia  mirathi na mambo ya kifamilia.,
 Aidha  hatua  hiyo, itasaidia  kuwawezesha   makundi maalum ambayo  wanawake na watoto wakiwemo na wasimamizi wa mirathi  wanaohitaji  huduma hiyo kuendelea  kushiriki katika shughuli za maendeleo na kukuza uchumi wa nchi.
 Kauli hiyo ilitolewa jana na Mwenyekiti wa Mkutano wa Mashauriano kuhusu  uanzishaji   Kituo  Maalum cha  kushughulikia masuala ya mirathi, ambaye ni Msajili ya Mahakama Kuu ya Tanzania,Mhe. Ilvin Mugeta kwenye ukumbi wa mikutano wa Tume ya Kurekebisha  Sheria,uliopo  Jijini Dar es Salaam.
“Tuna  mapango wa kuanzisha  kituo hicho cha  huduma  za Mahakama   kuhusiana  na masuala  ya mirathi, ambacho  kitakuwa na wadau  mbalimbali wa Mahakama  ya Tanzania ili  kuhakikisha  huduma za mirathi zinatolewa kwa wakati  bila kupoteza muda  na gharama,” alisema Mwenyekiti huyo.
Aliongeza kwamba kituo hicho kitaanzishwa   katika jiji la Dar es Salaam, ikiwa ni mradi wa mfano, lakini baadae  vitaanzishwa katika mikoa mingine.
 Aidha   Mhe. Mugeta   ambaye pia alikuwa mgeni rasmi  katika mkutano huo, alisema kituo hicho, kitaanzishwa  katika jiji hilo kwa  sababu  tatizo hilo, kubwa kwa sababu   lina wakazi wengi.
Aliitaja  sababu  ya kuanzishwa kituo hicho, kimetokana  kwamba Mahakama ya Tanzania huwa inapokea maoni 3,000 kila siku  kuhusiana na masuala hayo.
“Kituo hicho kitakuwa na huduma za Mahakama za Mwanzo, Wilaya na Mahakama Kuu, ili kuweza kuondoa vipingamizi  katika utoaji wa huduma hizo.
Alisema  katika kituo hicho,  kinatarajiwa  kuwa  na  huduma za  utoaji wa vyeti vya kuzaliwa na cheti kifo, huduma za mifuko ya hifadhi ya jamii  na kibenki.
Baadhi ya wadau  wa mkutano huo, walipendekeza kwamba elimu zaidi  itolewe kuhusiana na masuala ya mirathi.
Mkutano huo, ambao umeandaliwa na Mahakama ya Tanzania, umewashirikisha  baadhi ya viongozi wa Mahakama  na wadau mbalimbali  ambao ni  Chama  cha Wanasheria Wanawake  Tanzania, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, ambayo ni (NSSF), (PSPF),  Mamlaka  ya Usimamia  Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Chama  cha Mawakili Tanganyika(TLS) na Baraza Kuu la Waislaamu Tanzania(BAKWATA).
caption  ya picha

Picha  ya Baadhi ya  wadau  wa   Mkutano wa Mashauriano kuhusu  uanzishaji   Kituo  Maalum  cha  kushughulikia masuala ya mirathi , wakiwa  katika  picha ya  pamoja  kwenye ukumbi wa mikutano wa Tume ya  Kurekebisha  Sheria,uliopo  Jijini Dar es Salaam.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni