SERIKALI YAPONGEZWA KWA KILIPA DENI LA MIFUKO YA HIFADHI ZA JAMII




 MFUKO wa hifadhi ya wafanyakazi wa serikali za mitaa,LAPF,umeipongeza serikali kwa kulipa malimbikizo ya madeni ambayo mfuko huo na mingine ilikuwa ikiidai kwa miaka mingi na hivyo kuathiri usitawi wa mifuko hiyo..

Meneja wa LAPF kanda ya kaskazini, Rajabu Kinande, amesema hatua ya serikali kulipa madeni hayo kumeiongezea mifuko ya hifadhi ya jamii uwezo wa kuhudumia wanachama wao kwa wakati. 

Kinande, ameyasema hayo Marchi 7  jijini Arusha,alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari kwenye kituo cha mikutano ya kimataifa, AICC, kuelezea hatua ya maandalizi ya mkutano mkuu wa siku mbili wa mwaka wa wadau wa LAPF.
Amesema mkutano huo  utafunguliwa na Waziri mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania,Mh,Majaliwa Kassim Majaliwa,Marchi 9 mwaka huu ambapo zaidi ya wanachama 1000 wa mfuko huo wanatarajiwa kuhudhuria.
Awali Meneja Mawasiliano na Masoko wa LAPF,James Mloe, amesema kuwa kwenye mkutano huo kutawasilishwa mada mbalimbali zikiwemo Uendeshaji wa shughuli za mfuko huo,Hesabu zilizokaguliwa na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali(CAG)za mwaka 2015/16 ambapo mfuko huo umepata hati safi ya ukaguzi wa hesabu  ,UKusanyaji wa michango  ulipaji wa mafao kwa wanachama na uwekezaji ,Utawala bora  na usimamizi wa uendeshaji wa mfuko huo na Raslimali fedha .
Amesema siku ya kwanza ya mkutano huo Marchi 9 kwa kuzingatia kuwa ni siku ya Figo duniani mfuko umeandaa upimaji wa figo bure kwa wanachama wote ambao utafanywa na Madaktari bingwa.
 .Mloe,amesema siku ya pili ya mkutano huo Waziri mkuu Kassim Majaliwa atazindua  program mpya ya mikopo kwa wanachama kwa kushirikiana na benki ya CRDB, iitwayo Maisha popote  ambao ni mkopo wa kwanza kutolewa na mfuko huo.
Amesema kauli mbiu ya mwaka huu ni kuibua fursa endelevu za ajira  kwa maendeleo endelevu kwa watanzania.
Kuhusu uwekezaji kwenye viwanda,Mloe, amesema kuwa LAPF, imeweka  mitaji kwenye viwanda  ambako tayari wameweka hisa zao .
Amesema kuwa LAPF,haiwezi kujenga viwanda na kuvisimamia uendeshaji wake bali itaweka mitaji na kusisitiza kuwa LAPF itabakia kwenye jukumu lake la msingi la kulinda michango ya wanachama wake.
  Mwisho .

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni