Rais
 wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) Anthony Mtaka akikabidhi Bendera 
kwa manahodha wa timu ya taifa ya riadha kwa upande wa wanaume,Fabian 
Joseph (kushoto) na Magdalena Shauri (kulia)Wengine ni Kaimu Mkurugenzi 
wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Nyamakumbati Mafuru (mwenye 
miwani) ,Meneja Mawasiliano wa TANAPA,Pascal Shelutete na kushoto ni 
Meneja wa timu ya taifa ya riadha Meta Petro.
Raisi
 wa Shirikisho la Riadha Tanzania ,Anthony Mtaka akizungumza na 
wanariadha 28 wanaoelekea nchini Uganda kwa ajili ya Mashindano ya Dunia
 ya Mbio za Nyika wakati wa hafla fupi ya kuwaaga iliyofanyika katika 
ofisi za Makao Makuu ya TANAPA jijini Arusha.
Kaimu
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Nyamakumbati 
Mafuru akitoa neno kwa wanariadha hao,Shirika la Hifadhi za Taifa ndilo 
limedhamini wanariadha hao ambao idadi yao katika ushiriki wa mbio hizo 
imevunja rekodi ya tangu mwaka 1991.
Baadhi ya wanariadha watakao iwakilisha nchi katika mashindano hayo yatakayofanyika jumapili hii.
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) Whilleam Gidabuday akizungumza wakati wa hafala hiyo.
Meneja
 Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Pascal Shelutete 
akizungumza wakati wa hafla ya kuwaaga wanariadha wa timu ya taifa 
iliyoandaliwa na shirika hilo jijini Arusha.
Kikosi
 cha wanariadha 28 na viongozi 12 kitakachopeperusha Bendera ya Taifa 
nchini Uganda katika Mashindano ya Dunia ya Mbio za Nyika 
yatakayofanyika Jumapili hii katika mji wa Entebe.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni