RAIS TRUMP AKERWA NA MKWEWE NA BINTI YAKE KUWA MAPUMZIKONI WAKATI HUU MUHIMU


Rais Donald Trump ameripotiwa kukasirishwa na kitendo cha mkwewe ambaye ni mshauri wake mwandamizi pamoja na binti yake kuwa katika mapumziko wakati wa kura muhimu ya ya muswada wake wa afya.

Binti yake huyo Ivanka Trump na mumewe Jared Kushner wapo huko Aspen pamoja na watoto wao wakifurahia mapumziko yao kwa kucheza mchezo wa kuteleza kwenye barafu, wakati wa maamuzi muhimu ya muswada huo.

Muswada huo wa afya wa Marekani, umeshindwa kupita katika baraza la Congress licha ya kuwa na wawakilishi wengi wa Republican, ambapo Spika Paul Ryan alilazimika kuuondoa jana.
                    Ivanka Trump akiwa na mumewe Jared Kushner mapumzikoni huko Aspen
           Ivanka Trump na mumewe Jared Kushner wakiteleza kwenye barafu huko Aspen

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni