FEDHA ZA MWANAMUZIKI JAGUAR ZA SABABISHA KIFO CHA MTU

Polisi nchini Kenya wanachunguza tukio la mtu mmoja kuuwa na kundi la watu baada ya kunyakua fedha ambazo zinadaiwa zilitolewa na mwanamuziki, Charles Kanyi aka Jaguar.

Mwanamuziki Jaguar ameshatangaza nia ya kuwania ubunge katika jimbo la Ziwani, na wakati tukio hilo alikuwa Ziwani kwenye kampeni na alitoa fedha kwa kundi la vijana.

Kwa mujibu wa mashuhuda na polisi, kiongozi wa kundi hilo alinyakua fedha hizo na kukimbia na ndipo wenzake walipomkimbiza na kisha kumpiga hadi kufa.

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nairobi, Japheth Koome, amesema bado wanaendelea na uchunguza tukio hilo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni