Na Felix Mwagara/MOHA   
NAIBU
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amelitaka 
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kuanzisha kituo cha zimamoto Wilaya ya 
Ruangwa mkoani Lindi.   
Masauni
 alisema Aprili Mosi mwaka huu Jeshi hilo litakuwa na ofisi wilayani 
humo ili askari wa Jeshi hilo waanze kutoa huduma sehemu mbalimbali ya 
Wilaya hiyo ambayo ni muhimu kituo hicho kuwepo kutokana na uwepo na 
machimbo ya madini ya dhahabu pamoja na mji kuendelea kukua kwa kasi.    
“Tumekubaliana
 vizuri baada ya Kamanda wa Zimamoto mkoa kuwa ifikapo tarehe moja 
askari wa zimamoto watakuwepo hapa Ruangwa rasmi kwa ajili ya kuanza 
kazi, na watapewa ofisi na halmashauri ya Wilaya, hivyo utaratibu wa 
kupata vifaa vya awali uanze mara moja kama tulivyokubaliana,” alisema 
Masauni. 
Kwa
 upande wake Kamanda wa Jeshi hilo Mkoa wa Lindi, Christina Sunga 
alimuhakikishia Naibu Waziri pamoja na Watendaji wa Wilaya hiyo, agizo 
hilo atalifanyia kazi haraka iwezekanavyo na mpaka ifikapo Aprili mosi 
mwaka huu tayari askari wawili watakuwa wameripoti mjini Ruangwa.    
“Uwepo
 wa askari hawa kutarahisisha kwa kiasi kikubwa kutoa elimu kwa umma 
jinsi ya kuzima moto pamoja na kupambana na uzimaji moto, licha ya kuwa 
tunakuwa na vifaa vya awali vya uzimaji moto mpaka hapo tutakapopata 
gari kwa ajili ya shughuli mbalimbali za uzimaji moto na utoaji elimu 
zaidi,” alisema Sunga na kuongeza;    
“Tunashukuru
 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa kwa kutupa ofisi kwa ajili ya askari 
wa zimamoto lakini pia kutuwezesha kupata vifaa hivyo vya awali vya 
uzimaji wa moto.”   
Aidha,
 Masauni alimuagiza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, (RPC) Renatha 
Mzinga kuandaa mchoro pamoja na gharama ya ujenzi wa kituo kikubwa cha 
polisi cha Wilaya ya Ruangwa ili ujenzi huo uanze.    
“Nimekagua
 eneo la ujenzi wa kituo kipya cha polisi, eneo zuri na linafaa kwa 
ujenzi wa kituo kikubwa cha polisi, maandalizi tayari yameanza na hivi 
karibuni RPC atakamilisha mchoro pamoja na gharama ya ujenzi wa kituo 
hicho hapa Ruangwa,” alisema Masauni.    
Pia
 Masauni amesema Wizara yake itahakikisha inawajengea ofisi Uhamiaji, 
Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida) pamoja na Jeshi la Zimamoto na 
Uokoaji wilayani humo ambapo kwasasa ofisi hizo zipo katika jengo la 
Halmashauri ya Wilaya hiyo.   
Naibu
 WaziriMasauni amemaliza ziara yake ya siku mbili kwa kutembelea miradi 
mbalimbali ya maendeleo pamoja na kuzungumza na askari na maafisa wa 
vyombo walio chini ya wizara yake mkoani Lindi na tayari amesafiri 
mkoani Mtwara kuendelea na ziara yake.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni