MTU MMOJA AUAWA AKIDHANIWA KUWA NI MWIZI WA PIKIPIKI .


Na.Mahmoud Ahmad ,Arusha.

Mtu moja ambaye jina lake hajijafahamika ameuawa na wananchi wenye hasira  kali huko maeneo ya kwa Mrombo Jijini Arusha ,akidhaniwa kuwa ni mwizi wa pikipiki baada ya mtu huyo kupita na kufananishwa na waendesha pikipiki hao.

Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Charles Mkumbo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo  ambapo amesema kuwa  majira ya saa saba mchana wananchi hao walimuona mtu huyo wakadania kuwa ndiye aliyewahi kumnyanyanya  mwenzao pikipiki hivyo wakaanza kumshambulia na kumburuza ambapo hadi jeshi la polisi kufika eneo la tukio mtu huyo alikuwa tayari ameshachoka na hali yake ilikuwa mbaya wakiwa njiani kumpeleka hospitali alifariki.

Kamanda Charles Mkumbo amewataka wananchi kutochukua sheria mkononi kwani wanaweza kumdhuru mtu ambaye hausiki na tukio amesema kuwa wanapomuhisi mtu kuwa ni muhalifu watoe taarifa kwa jeshi la polisi ili sheria ichukue mkondo wake. 

Hadi sasa jeshi la polisi mkoani hapa linawashikilia watu watano ambao ni waendesha pikipiki kwa kuhusika katika tukio hilo,mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya maountmeru ukisubiria ndugu na jamaa kwenda kumtambua.




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni