Serikali
 inajipanga kwajili wataalamu wa maendeleo ya jamii 5,554 kwa kipindi 
cha miaka mitano ili waweze kutoa huduma za maendeleo ya jamii 
kuanzia  ngazi ya Serikali kuu hadi kijiji kama ilivyokuwa kwa utawala 
wa awamu ya kwanza nchini.
Ameyasema hayo katika Mahafali ya sita ya Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tenguru nje
 kidogo ya jiji  la Arusha Naibu Waziri Wizara ya Afya, Maendeleo ya 
Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Hamis Kigwangalla amesema serikali ya 
awamu ya kwanza ilikuwa na idadi kubwa ya mabibi na mabwana maendeleo ya
 jamii kila kata.
 Aliongeza kuwa kwasasa wataalamu katika sekta ya maendeleo ya jamii  wameanza
 kupungua sana na kukitaka chuo kuongeza udaili wa wanafunzi ili 
kuendana na azima ya serikali ya kuwa na wataalamu awa kila wilaya na 
kata.
Aidha
 aliitaka Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru kuendela kutoa taaluma 
yenye viwango na  bora na uzingatiwe katika mchakato wote wa utoaji 
mafunzo kuanzia kwenye udahili wa wanafunzi wenye sifa na vigezo ili 
kujenga jamii ya wasomi wenye tija katika Taifa letu
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni