UMOJA
 wa Ulaya (EU) na Umoja wa Mataifa (UN) wamejiunga pamoja kuendesha 
kampeni ya uelewa wa malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) nchini 
Tanzania . Aidha kwa pamoja wamezuru miradi iliyofadhiliwa na EU. Wakiwa
 Mkoani Iringa wamepata nafasi ya kuzungumza na wanachuo 1,000 kutoka 
vyuo vikuu vya Iringa na Mkwawa kwenye semina iliyoelezea malengo hayo 
ya dunia ambayo ni sehemu ya ajenda 2030 ya maendeleo endelevu duniani. 
Kampeni hiyo imelenga kuwafanya vijana waelewe malengo 17 ya dunia 
ambayo kwa sasa yana mwaka mmoja tangu yapitishwe na kuwatanabaisha 
wajibu wao katika kufanikisha utekelezaji wake ndani ya mazingira ya 
Tanzania.  
Mwakilishi
 wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro 
(kushoto) akisalimiana na mmoja wa wahadhiri wa chuo hicho alipowasili 
katika ofisi za Mkuu wa Chuo Kikuu cha Iringa (UOI), Prof Joshua 
Madumulla akiwa ameambatana na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa 
Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa
 (UNDP), Alvaro Rodriguez.(Picha zote na Zainul Mzige wa Moblog)
Semina
 katika vyuo hivyo ni sehemu ya mpango madhubuti wa Umoja wa mataifa 
uliozinduliwa Arusha Mei mwaka huu na Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa 
Mataifa, Bw. Alvaro Rodriguez wenye lengo la kuwaelimisha vijana zaidi 
ya 30,000 ifikapo mwaka ujao kuhusu malengo hayo ya dunia. Ujumbe huo wa
 EU na UN pia ulipata nafasi ya kutembelea miradi mbalimbali 
inayofadhiliwa na EU ukiwamo wa Boma la Kijerumani ambalo lilikarabatiwa
 kwa ruzuku ya EU kupitia 'fahari yetu – Southern Highlands Culture 
Solutions'. Boma hilo ni moja ya majengo ya zamani katika mji wa Iringa 
na lilijengwa na Wajerumani mwaka 1900 kama hospitali ya kijeshi. Baada 
ya vita ya Kwanza ya Dunia, jengo hilo lilibadilishwa matumizi na 
watawala wapya, Uingereza, na kulifanya kuwa jengo la utawala. EU 
imesema inaona fahari kuwa mmoja wa wawekezaji wakubwa katika sekta ya 
sanaa na urithi wa kitamaduni nchini Tanzania, ikifadhili miradi 10 
iliyo chini ya programu ya 10 ya EDF ya kusaidia masuala ya kitamaduni. 
 
Mkuu
 wa Chuo Kikuu cha Iringa (UOI), Prof Joshua Madumulla akiwa kwenye 
mazungumzo na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na 
Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro 
Rodriguez aliyeambatana na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini 
ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro (upande wa kushoto katikati) 
pamoja na Mtaalam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa Tanzania, Hoyce 
Temu (kushoto) alipotembelewa ofisini kwake na ugeni huo. Kulia ni 
Meneja wa Mradi wa Fahari Yetu, Jan Kuever pamoja na Katibu Tawala 
Msaidizi -Miundombinu wa Mkoa wa Iringa, Henry Mditi.
Masuala
 yanayohusu urithi wa kitamaduni ni muhimu katika kuchagiza ukuaji wa 
uchumi, ajira na huku ikifuma mahusiano ya kijamii, na kutoa fursa ya 
kuboresha utalii endelevu mkoani Iringa huku ikileta faida kwa wakazi wa
 eneo hilo. Bw. Rodriguez, akizungumza katika kampeni hiyo alisema 
kwamba ajenda 2030 ambayo ni ajenda ya maendeleo endelevu inahitaji 
ushiriki wa kila mmoja.Aliwapongeza wanachuo hao na wanazuoni kwa 
kujikita kutambua malengo hayo ya dunia. Aidha aligusia umuhimu wa 
vijana kushiriki katika masuala ya maendeleo kutokana na ukweli kuwa, 
kwa taifa kama la Tanzania vijana ni asilimia 60 ya wananchi wote 
waliopo.Alisema kwamba vijana wanajukumu kubwa la kushiriki katika 
maendeleo hayo kwa lengo la kuipeleka nchi katika hatua nyingine ya 
maendeleo. 
 
Mratibu
 Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika 
la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akiwa 
ameongozana na Katibu Tawala Msaidizi -Miundombinu wa Mkoa wa Iringa, 
Henry Mditi kuelekea kwenye ukumbi wa mikutano Chuo Kikuu cha Iringa.
Hata
 hivyo alisema kwamba ni wajibu wa kila mtu hasa vijana, kuhakikisha 
kwamba malengo hayo ya dunia yanafanikiwa . Alisema Umoja wa Mataifa kwa
 kusaidiwa na wadau wake muhimu kama Umoja wa Ulaya, utaendelea kusaidia
 Watanzania kuwajibika katika shughuli mbalimbali za maendeleo katika 
kuunga mkono malengo hayo ya dunia. Mmoja wa washiriki alipongeza Umoja 
na wa Mataifa kwa kuwafikia vijana wa vyuoni na kuwapa semina hiyo. 
“Ninajisikia mtu mwenye bahati kupata nafasi ya kujifunza maendeleo 
endelevu kutoka kwa Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini. 
Nikiwa kama kijana, naona faraja kuona kwamba viongozi wetu wanafuata 
maelekezo yaliyofafanuliwa kwenye malengo 17 ya maendeleo endelevu; 
naamini kama tukijitahidi kuyafikia ifikapo 2030, basi Tanzania na 
duniani kwa ujumla itakuwa eneo jema la kuishi. Na kwa kuwa sasa 
natambua kuhusu malengo hayo ya dunia, ninaweza kutoa mchango wangu 
kusaidia kuyafikia -najisikia kuwezeshwa sana.” amesema Mary, mmoja wa 
washiriki. 
 
Mkuu
 wa Chuo Kikuu cha Iringa (UOI), Prof Joshua Madumulla akisoma taarifa 
fupi ya Chuo Kikuu cha Iringa mbele ya ujumbe kutoka Umoja wa Mataifa na
 Umoja wa Ulaya wakati semina kuhusu malengo ya Maendeleo Endelevu 
(SDGs) ambayo ni sehemu ya ajenda 2030 ya maendeleo endelevu duniani kwa
 wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa.
Mkuu
 wa wilaya ya Iringa, Richard Kasesela akizungumza kwenye semina ya 
malengo ya dunia kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa ambapo aliwaasa 
wakawe mabalozi wazuri wa malengo hayo kwenye jamii zao na wanafunzi 
wenzao wa vyuo vingine.
Mwakilishi
 wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro 
akitoa salamu za Umoja wa Ulaya kwa niaba ya Balozi wa Umoja huo, Bw. 
Roeland Van De Geer wakati wa semina Malengo ya Maendeleo Endelevu 
(SDGs) kwa wanachuo wa Iringa iliyowezeshwa na EU.
Mratibu
 Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika 
la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akiwapiga 
msasa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa kuhusu Malengo ya Dunia katika 
semina iliyofadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU) mjini Iringa.
Mwanafunzi
 wa mwaka wa tatu anayechukua Shahada ya Sayansi katika Uchumi na Fedha 
wa Chuo Kikuu cha Iringa, Sarafina Sayi akiuliza swali kwa mkufunzi wa 
malengo ya dunia Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini 
na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro
 Rodriguez (hayupo pichani) wakati wa semina hiyo.
Mwanafunzi
 wa Shahada ya Sayansi katika Uchumi na Fedha wa Chuo Kikuu cha Iringa, 
Geoffrey Kadori akiuliza swali kwa Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard 
Kasesela wakati wa semina ya Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) ambayo
 ni sehemu ya ajenda 2030 ya maendeleo endelevu duniani kwa wanafunzi wa
 Chuo hicho.
Mkuu
 wa wilaya ya Iringa, Richard Kasesela akijibu swali wakati wa kipindi 
cha maswali na majibu kwenye semina kuhusu malengo ya maendeleo endelevu
 (SDGs) kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa.
Pichani
 juu na chini ni wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa kutoka vitivo 
tofauti chuoni hapo waliohudhuria semina ya malengo ya Maendeleo 
Endelevu (SDGs) ambayo ni sehemu ya ajenda 2030 ya maendeleo endelevu 
duniani kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa iliyofadhiliwa na Umoja 
wa Ulaya (EU).
Mratibu
 Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika 
la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akimkabidhi 
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Iringa (UOI), Prof Joshua Madumulla makabrasha na
 majarida yenye ripoti na taarifa mbalimbali za Umoja wa Mataifa.
Mratibu
 Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika 
la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akimkabidhi 
Mkuu wa wilaya ya Iringa, Richard Kasesela ripoti na makabrasha 
mbalimbali ya Umoja wa Mataifa mara baada ya kuhitimisha semina kuhusu 
SGDs kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa.
Mkuu
 wa wilaya ya Iringa, Richard Kasesela (wa tatu kulia) katika picha ya 
pamoja na ujumbe kutoka Umoja wa Mataifa, Umoja wa Ulaya pamoja na 
Balozi wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs Champion), Sabinus Paul 
(kushoto) nje ya ukumbi kulikofanyika semina kuhusu SDGs kwa wanachuo wa
 Iringa.
Picha ya pamoja na sehemu ya washiriki wa semina hiyo huku wakiwa na mabango ya SDGs.
Muonekano
 wa nje wa jengo la Makumbusho ya Mkoa na Kituo cha Utamaduni -Iringa 
Boma ambalo limejengwa kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU).
Kibao cha Makumbusho ya Mkoa wa Iringa kinachoratibiwa na Mradi wa Fahari yetu kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Iringa
Meneja
 wa Mradi wa Fahari Yetu, Jan Kuever akielezea dhumuni la mradi Fahari 
Yetu unaolenga kuendeleza utamaduni nyanda za juu kusini kwa Mratibu 
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika 
la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez (wa pili 
kushoto) aliyeambatana na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini 
ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro (mwenye suti) ambao ndio wafadhili
 wa jengo hilo la Makumbusho ya Mkoa wa Iringa. Wengine katika picha ni 
wahadhiri na maprofesa kutoka Chuo Kikuu cha Iringa.
Mratibu
 Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika 
la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akisaini 
kitabu cha wangeni ndani ya Makumbusho ya mkoa wa Iringa.
Mwakilishi
 wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro 
akisaini kitabu cha wageni alipowasili katika Makumbusho ya mkoa wa 
Iringa.
Meneja
 wa Mradi wa Fahari Yetu, Jan Kuever akitoa maelezo picha mbalimbali 
zinazoelezea historia ya mkoa wa Iringa wakati wa utawala wa Chifu 
Mkwawa kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na 
Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro 
Rodriguez aliyeambatana na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini 
ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro walipotembelea makumbusho ya mkoa 
wa Iringa
Mratibu
 Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika 
la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akisoma 
historia mbalimbali za enzi za utawala wa kichifu ndani ya Makumbusho ya
 Mkoa wa Iringa.
Mwongoza
 wageni katika Makumbusho ya mkoa wa Iringa, Jacob Shenyagwa (mwenye 
miwani) akitoa maelezo ya picha mbalimbali kwa ugeni huo wa UN na EU 
uliotembelea makumbusho hiyo iliyojengwa chini ya ufadhili wa Umoja wa 
Ulaya (EU).
Mwongoza
 wageni katika Makumbusho ya mkoa wa Iringa, Deonis Mgumba akitoa 
maelezo ya vifaa mbalimbali vilivyokuwa vikitumika enzi za utawala wa 
kichifu kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na 
Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro 
Rodriguez (kushoto) na Katibu Tawala Msaidizi -Miundombinu wa Mkoa wa 
Iringa, Henry Mditi (katikati) walipotembelea makumbusho hayo mjini 
Iringa.
Mratibu
 Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika 
la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez na Mwakilishi 
wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro 
wakitwanga mahindi kienyeji katika moja ya kinu kilichokuwa kinatumika 
enzi hizo za utawala wa kichifu kilichopo katika makumbusho hayo.
Mwongoza
 wageni katika Makumbusho ya mkoa wa Iringa, Matatizo Kastamu akitoa 
maelezo ya picha mbalimbali zenye kumbukumbu za utawala wa kichifu na 
historia ya mji wa Iringa kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa 
Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa
 (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya 
(EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro.
Mwakilishi
 wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro 
(kushoto), Mtalaam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu
 na Meneja wa Mradi wa Fahari Yetu, Jan Kuever wakipitia vipeperushi 
vyenye maelezo ya kina ya Mradi wa Fahari Yetu unaoendesha Makumbusho na
 Kituo cha Utamaduni mkoa wa Iringa.
Mratibu
 Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika 
la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez na Mwakilishi 
wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro 
katika picha ya pamoja kwenye sanamu maalum za mavazi ya kipindi cha 
utawala wa Chifu Mkwawa walipotembelea Makumbusho ya mkoa wa Iringa.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni