Waziri
 wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati), akijadiliana
 jambo na Waziri wa Nishati wa Zambia, David Mabumba (kushoto) na 
Mkurugenzi kutoka Bomba la Mafuta la TAZAMA, D. Legge (kulia).
 Waziri
 wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (Kulia), na Waziri wa 
Nishati wa Zambia, David Mabumba wakifurahia jambo mara baada ya 
mazungumzo baina yao yaliyofanyika Ofisini kwa Waziri Muhongo jijini Dar
 es Salaam.
 Waziri
 wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) na Waziri wa 
Nishati wa Zambia, David Mabumba (wa tatu kutoka kushoto), wakiwa katika
 picha ya pamoja na Ujumbe ulioambatana na Waziri Mabumba. Wa Tatu 
kutoka Kulia ni Kaimu Katibu Mkuu, Profesa James Mdoe.
 Waziri
 wa Nishati wa Zambia, David Mabumba (kushoto) akimuaga Waziri wa 
Nishati na Madini nchini, Profesa Sospeter Muhongo (wa pili kutoka 
kushoto) baada ya kikao chao kilichofanyika ofisini kwa Waziri Muhongo. 
Wa pili kutoka Kulia ni Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara, Profesa James Mdoe 
akiagana na Mkurugenzi kutoka Bomba la TAZAMA, D. Legge.
 Waziri
 wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (wa pili kutoka kulia) 
akizungumza na Waziri wa Nishati wa Zambia David Mabumba (wa tatu kutoka
 kulia) na Ujumbe wake, ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Waziri
 wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, akisisitiza jambo 
wakati wa kikao chake na Waziri wa Nishati wa Zambia, David Mabumba na 
Ujumbe wake (hawapo pichani) walipomtembelea ofisini kwake jijini Dar es
 Salaam.
Na Veronica Simba.
Waziri
 wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na Waziri wa Nishati wa 
Zambia, David Mabumba, wamekutana na kufanya mazungumzo kuhusu kuboresha
 Bomba la Mafuta la TAZAMA ili liweze kuwanufaisha wananchi wa Tanzania 
na Zambia kama ilivyokusudiwa.
Mazungumzo
 yao yaliyofanyika mapema leo, ofisini kwa Waziri Muhongo jijini Dar es 
Salaam, ni kufuatia makubaliano ya marais wa nchi husika, Dk John 
Magufuli na Edgar Lungu; kuhusu kuboresha zaidi Bomba la TAZAMA na Reli 
ya TAZARA.
Marais
 Magufuli na Lungu, walifikia makubaliano hayo jana katika mazungumzo 
rasmi yaliyofanyika Ikulu ya Dar es Salaam ambayo ni mojawapo ya 
shughuli mbalimbali zilizopangwa katika ratiba ya ziara ya siku Tatu (3)
 ya Rais Lungu iliyoanza nchini Jumapili, Novemba 21 mwaka huu. 
Waziri
 Mabumba ambaye alifuatana na Ujumbe wa Viongozi na Maafisa waandamizi 
kutoka TAZAMA na wizarani kwake; aliafiki mapendekezo yaliyotolewa na 
Waziri Muhongo kuhusu namna pande hizo mbili zitakavyoshirikiana katika 
utekelezaji wa agizo la Marais wao ambayo ni pamoja na wataalam wa pande
 zote kukutana na kufanya majadiliano pamoja na kufanya ziara kukagua 
utendaji kazi wa Bomba hilo.
Aidha, Mawaziri hao walijadiliana kuhusu namna ambavyo Zambia itanufaika na gesi asilia iliyogunduliwa Kusini mwa Tanzania. 
Kikao
 hicho pia, kilihudhuriwa na viongozi waandamizi wa Wizara ya Nishati na
 Madini – Tanzania, akiwamo Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara, Profesa James 
Mdoe.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni