NDEGE YAANGUKA NA KUUWA WATU WAKIWEMO WACHEZAJI WA TIMU YA BRAZIL

Ndege ya abiria ikiwana watu 81, wakiwemo wachezaji wa timu ya Chapecoence ya Brazil imeanguka katika mji wa Medellin nchini Colombia.

Ndege hiyo imeanguka wakati ikikaribia mji huo baada ya kupata hitilafu katika mfumo wa umeme, ambapo taarifa zinasema watu sita wamenusurika kifo.

Wachezaji hao wa timu ya Chapecoence walikuwa wanaenda katika mchezo wa fainali ya Copa Sudamericana, dhidi ya timu ya Medellin ya Atletico Nacional.
Viongozi na wachezaji wa timu ya Chapecoence wakiwa kwenye ndege hiyo kabla ya kuanguka

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni