USAIN BOLT AZINDUA FILAMU YAKE YA 'I AM BOLT' NCHINI UINGEREZA


Mwanariadha nyota Mjamaica Usain Bolt ambaye pia ni mshindi wa medali ya dhahabu mara tisa katika michuano ya Olimpiki amezindua filamu yake ya 'I Am Bolt' nchini Uingereza.

Uzinduzi huo umefanyika ODEON Leicester Square na kuhudhuriwa na nyota kadhaa maarufu wa soka kama vile Hector Bellerin na Nacho Monreal wa Arsenal na Cesc Fabregas wa Chelsea.

Wengine waliohudhuria uzinduzi wa filamu hiyo ni Raheem Sterling, Mo Faraha, Olivier Giroud na mkewe, mchezaji wa zamani wa Arsenal Robert Pires pamoja na bondia David Haye. 
Mwanariadha Usain Bolt akiongea na waandishi wa habari waliofika katika uzinduzi wa filamu yake

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni