MCHUNGAJI ANAYEWAPULIZIA DAWA YA MBU WAUMINI ALALAMIKIWA



Jamii nchini Afrika Kusini imemlalamikiwa vikali Mchungaji mmoja nchini humo ambaye anawapulizia dawa ya mbu waumini wake wenye matatizo mbalimbali.

Akitumia ukurasa wake wa Facebook Mchungaji huyo anayejiita Mtume Lethebo Rabalago, amedai kuwa dawa ya mbu ya Doom inauwezo wa kufanya uponyaji.

Kampuni inayozalisha Doom imeonya juu ya madhara ya kumpulizia mtu dawa hiyo na tume ya serikali imewataka waumini waliodhurika kufungua malalamiko dhidi ya Mchungaji huyo.

Hata hivyo Mchungaji huyo wa kanisa la Mount Zion General Assembly katika mkoa wa Limpopo amejitetea kuwa anatumia miujiza kutibu watu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni